Habari za Punde

Maeneo 17 Dar Kufungwa CCTV Kamera


 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu, akiongoza Kikao cha wadau kutoka Taasisi mbalimbali za Serikali, kujadili Mradi wa kuweka Kamera za Kudhibiti Uhalifu(CCTV Kamera) katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dodoma.
Washiriki wa Kikao cha Wadau wa kujadili Mradi wa Kuweka Kamera za Kudhibiti Uhalifu(CCTV Kamera) katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam,Faraji Ntembo na Faizer Mbange(kushoto), wakipitia moja ya nyaraka inayohusu mradi huo wakati wa kikao hicho kilichoongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Jacob Kingu. Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dodoma.
Mshiriki wa Kikao cha Wadau wa kujadili Mradi wa Kuweka Kamera za Kudhibiti Uhalifu (CCTV Kamera) katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam,Wankyo Nashon akichangia hoja, kushoto  ni mshiriki Lina Rujweka. Kikao hicho kimefanyika  leo  jijini  Dodoma.
 Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.