Habari za Punde

UVCCM Mkoa wa Tanga Yawataka Vijana Kujitokeza Kuwania Nafasi za Uongozi Kwenye Chaguzi Zijazo.

Katibu wa Hamasa na Chipukizi Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga Waziri Mohamed

VIJANA mkoani Tanga wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuwania nafasi mbalimbali kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu na ule wa wabunge na madiwani mwakani.

Wito huo ulitolewa leo na Katibu wa Hamasa na Chipukizi Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga Waziri Mohamed wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema lazima vijana waweze kuona umuhimu wa kujikita kwenye nafasi mbalimbali za uongozi ili kuweza kuwatumikia wananchi kwa uadilifu na uzalendo mkubwa .

“Kama Rais alivyofanya kuwaamini vijana kwenye teuzi mbalimbali hivyo nasi tujitokeze kwa wingi kwenye uchaguzi huo kuomba kugombea nafasi mbalimbali na tunaweza kupata fursa na kuweza kuwatumikia wananchi “Alisema .

Hata hivyo alisema wao kama Jumuiya ya Vijana watawahamasisha vijana ambao wanadhani wanasifa za kuwania nafasi hizo ili waweze kuchangamkia fursa hiyo muhimu kwa jamii.

Katika hatua nyengine Katibu huyo ametumia milioni 10 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya CCM kata ya Mlingano wilayani Muheza.

Alisema aliamua kufanya ujenzi huo baada ya kata hiyo haina ofisi  kwa kipindi kirefu na kulazimika kutumia maeneo mengine na hivyo ndipo alipoamua kufanikisha ofisi hiyo.

“Baada ya kuchaguliwa kuwa Katibu Mwenezi wa CCM Kata hiyo na baadae kuchaguliwa kuwa Katibu wa Hamasa na Chipukizi Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Tanga ndipo nilipoanza ujenzi huo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.