Habari za Punde

Mawaziri wa Biashara ya Tanzania na Zambia Wazungumzia Masuala ya Uwekezaji Katika Miundombinu ya Usafirishaji.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, akisisitiza jambo kwa Waziri Biashara na Viwanda, Chris Yaluma, kutoka Zambia kuhusu masuala ya uwekezaji katika miundombinu ya usafirishaji, wakati alipomtembelea katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe (kushoto), akijadiliana jambo na Waziri wa Biashara na Viwanda, Chris Yaluma (kulia) kutoka Zambia wakati alipomtembelea katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Biashara na Viwanda kutoka Zambia, Chris Yaluma, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, wakati alipomtembelea katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Biashara na Viwanda kutoka Zambia, Chris Yaluma, akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi wa Huduma za Uchukuzi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi), Aron Kisaka, wakati alipotembelea ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe, akiagana na Waziri Biashara na Viwanda, Chris Yaluma, kutoka Zambia mara baada ya kukutana na kujadili fursa za uwezekezaji nchini hususan sekta ya usafirishaji katika ofisi ndogo ya Wizara jijini Dar es Salaam.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.