Habari za Punde

SADC YAPANIA KUIMARISHA MIUNDOMBINU YA USAFIRISHAJI

Mkurugenzi wa Sekritarieti ya SADC (Miundombinu), Bi.Rosemary Makoena, akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani), kuhusu utekelezaji wa mpango mkakati wa kuboresha miundombinu katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika-SADC, mkutano ulifanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Sekritarieti ya SADC (Viwanda na Biashara), Bwana. Calicious Tutalife, akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani), kuhusu utekelezaji wa mpango mkakati wa kuboresha biashara  katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika-SADC, mkutano ulifanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi WA Sekritarieti ya SADC (Ulinzi na Usalama), Bwana. Jorge Cardoso, akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani), kuhusu historia ya ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika kuwekwa kwenye mitaala ya wanafunzi wa elimu ya msingi, mkutano ulifanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Na.Paschal.Dotto  - MAELEZO                                                                                                               
SEKRITARIETI ya Miundombinu ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika (SADC) inajikita katika kuimarisha na kuboresha miundombinu ya usafirishaji kwa kufanya ukarabati na kuhuisha sekta hiyo hususani sekta ya Bandari, Reli na Anga.                               

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Sekritarieti ya SADC Miundombinu Bi.Rosemary Makoe na amesema kuwa hakuna Maendeleo pasipo kuwa na uimarishwaji wa sekta hiyo, ili kuhakikisha kuwa nchi wanachama wanaunganishwa na sekta hiyo kufanyabiashara katika ukanda wao.

Ameongeza kuwa Miundombinu unayopigiwa chapuo kwenye utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Miaka 5 ni pamoja na Miundombinu ya Usafirishaji ambayo imebeba dhamira kubwa kwenye kuimarisha mawasiliano ya kibiashara baina ya nchi wanachama.

“Katika Mpango Mkakati wa 2015-2020 kwa nchi wanachama wa SADC tunaangalia zaidi kwenye utekelezaji na uangalizi wa miradi ya uimarishwaji wa miundombinu ya kusafirisha bidhaa. Mpango mkakati huo unalenga kuimarisha Sera mbali mbali ikiwemo ile ya uendelezwaji na ukarabati wa Bandari (SADC Corridors  of 2008) ya ukanda wetu wa kusini mwa Afrika”, Amesema Makoena.

Aidha, mpango huo wa SADC unalenga zaidi kwenye kusaini, kutekeleza na kuendeleza Sheria itakayozileta pamoja nchi wanachama katika kuendeleza sehemu za lango la usafirishaji wa majini. 

Hii itawezesha wananchi kwenye nchi hizo kufanyabiashara kwa urahisi bila vikwazo vyovyote.

Akisisitiza jambo hilo amasema kuwa mpango huo unaendana na makubaliano ya wanachama walioko katika bandari mbali mbali zilizoko katika ukanda huo wa kusisni mwa Afrika. Ikianzia bandari ya Mtwara, Dar esSalaam, Trans-Kalahari, Central Beira na Nacala ambapo wanachama wataweka kanuni kulingana na makubaliano yao ya usafirishaji yalifanyika chini ya Memorandum of Unederstanding For South-Northa amesema Makoena.
Alisema kuwa katika kuimarisha sekta hiyo ya usafirishaji wa majini, nchi wanachama walioko kwenye lango la bandari wanaweka kanuni, lengo, katiba na namna ya kuungana katika kuendeleza miradi ya ujenzi na ukarabati wa bandari hizo, ili kuboresha na kuhakikisha zinakuwa imara zaidi kwa kupokea mzigo ya kutosha.

“katika kutekeleza na kuhakikisha kuwa sekta hii inaimarika azma kubwa tuliyonayo sisi kama Sekritarieti ya Miundombinu ni kuboresha na kuhuisha sekta hii ili iweze kufanyakazi kwa ufanisi na uhakika zaidi. Sekritarieti inaendelea na mpango mkakati wa mwaka 2012-2021 na kuungwa mkono na Jumuiya ya Ulaya-EU ambao wako tayari kusaidia kuimarisha miundombinu katika nchi wanachama wa SADC”, Amesema Makoena.

Katika Mpango mkakati huo Sekritarieti ya Miundombinu inalenga zaidi katika kuimarisha na kuweka kanuni tisa (9) za pamoja kwa wanachama ikiwemo Udhibiti wa Uendeshaji wa magari ya mizigo barabarani, viwango na vipimo vya magari ya mizigo na mizani ya kupima magari yote, kwani kanuni hizo ni muhimu kwa usalama wa barabara na bidhaa.

Pia, Machi mwaka 2018 SADC ialisaini makubaliano ya Sheria ya usafirishaji wa kuvuka mipaka miongoni mwa nchi wanachama inayojulikana kama Cross-Border Road Transporter-Regulator Forum (CBRT-RF). Ambayo inafanyakazi pamoja na Transport and Transit Facilitation Program (TTFP) yenye kazi ya kusimamia mambo ya usafirishaji yote hayo ni kuhakikisha Sekta ya usafirishaji inakuwa imara katika Jumuiya hiyo.

Makoena aliongeza na kusema kuwa sekta ya usafirishaji kwa upande wa Anga inaimarishwa ili kuwezesha kuwepo na ndege kubwa za mizigo katika ukanda huo wa kusini mwa afrika. Kwani usafiri wa anga ni moja ya kichocheo muhimu katika kutekeleza ujenzi wa viwanda.

Hivyo, Sekritarieti ya Miundombinu inatekeleza hilo kwa kuanzisha Taasisi ya masuala ya usalama wa usafiri wa Anga (SADC Aviation Safety Organization, SASO) inayoshughulikia masuala ya usafiri wa anga katika nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.

Pamoja na hayo, SADC miundombinu inaendelea na utekelezaji wa ukarabati na ujenzi wa Reli katika Nchi wanachama ili kuimarisha na kulinda usalama wa barabara, kwani mizigo mizito itakuwa inasafarishwa kwa njia ya treni na kuepuka uharibu wa barabara.

Akimalizia Makoena alisema kuwa katika sekta ya Nishati SADC inajivunia utekelezwaji wa Mradi Mkubwa wa Ujenzi wa Bwawa la Umeme la Mto Rufiji nchini Tanzania, ambapo wanachama wa SADC watafaidika na umeme huo.

“Tunajivunia mradi huu, siyo SADC Jumuiya ya Afrika Mashariki-EAC, na tunakubaliana na kumuunga mkono kwa uongozi na mafanikio makubwa kwa Rais wa Sasa wa Tanzania katika utekelezaji wa mradi huo, tunahitaji kufanikisha hili kwa sababu tunahitaji Miundo mbinu hii. Amesema Makoena

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.