Mkurugenzi wa
Sekritarieti ya SADC (Miundombinu), Bi.Rosemary Makoena, akizungumza na
Waandishi wa Habari (hawapo pichani), kuhusu utekelezaji wa mpango mkakati wa
kuboresha miundombinu katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika-SADC,
mkutano ulifanyika katika Kituo cha Mikutano cha kimataifa Julius Nyerere
Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Sekritarieti
ya SADC (Viwanda na Biashara), Bwana. Calicious Tutalife, akizungumza na
Waandishi wa Habari (hawapo pichani), kuhusu utekelezaji wa mpango mkakati wa
kuboresha biashara katika Jumuiya ya
Maendeleo Kusini mwa Afrika-SADC, mkutano ulifanyika katika Kituo cha Mikutano
cha kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi WA Sekritarieti ya SADC (Ulinzi na Usalama),
Bwana. Jorge Cardoso, akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani),
kuhusu historia ya ukombozi wa nchi za kusini mwa Afrika kuwekwa kwenye mitaala
ya wanafunzi wa elimu ya msingi, mkutano ulifanyika katika Kituo cha Mikutano
cha kimataifa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Na.Paschal.Dotto - MAELEZO
SEKRITARIETI ya
Miundombinu ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini Mwa Afrika (SADC)
inajikita katika kuimarisha na kuboresha miundombinu ya usafirishaji kwa kufanya ukarabati na kuhuisha sekta hiyo hususani sekta
ya Bandari, Reli na Anga.
Akizungumza na Waandishi
wa Habari Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Sekritarieti ya SADC Miundombinu Bi.Rosemary Makoe na amesema kuwa hakuna Maendeleo pasipo kuwa na uimarishwaji
wa sekta hiyo, ili kuhakikisha kuwa
nchi wanachama wanaunganishwa na sekta hiyo kufanyabiashara katika ukanda wao.
Ameongeza kuwa
Miundombinu unayopigiwa chapuo kwenye utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Miaka 5 ni
pamoja na Miundombinu ya
Usafirishaji ambayo imebeba dhamira kubwa kwenye kuimarisha mawasiliano ya
kibiashara baina ya nchi wanachama.
“Katika Mpango Mkakati
wa 2015-2020 kwa nchi wanachama wa SADC
tunaangalia zaidi kwenye utekelezaji na uangalizi wa miradi ya uimarishwaji wa
miundombinu ya kusafirisha bidhaa. Mpango mkakati huo unalenga kuimarisha Sera mbali mbali ikiwemo ile
ya uendelezwaji na ukarabati wa Bandari (SADC
Corridors of 2008) ya ukanda wetu wa
kusini mwa Afrika”, Amesema Makoena.
Aidha, mpango huo wa
SADC unalenga zaidi kwenye kusaini, kutekeleza na kuendeleza Sheria itakayozileta pamoja nchi wanachama katika kuendeleza sehemu za lango la usafirishaji
wa majini.
Hii itawezesha wananchi kwenye nchi hizo kufanyabiashara kwa urahisi bila vikwazo vyovyote.
Akisisitiza jambo hilo amasema
kuwa mpango huo unaendana na makubaliano ya wanachama walioko katika bandari mbali mbali zilizoko katika ukanda huo
wa kusisni mwa Afrika. Ikianzia bandari ya Mtwara, Dar esSalaam, Trans-Kalahari, Central Beira na Nacala ambapo wanachama wataweka kanuni kulingana na makubaliano yao
ya usafirishaji yalifanyika chini ya Memorandum
of Unederstanding For South-Northa amesema Makoena.
Alisema kuwa katika kuimarisha sekta hiyo
ya usafirishaji wa majini, nchi wanachama walioko kwenye lango la
bandari wanaweka kanuni, lengo, katiba na namna ya kuungana katika kuendeleza miradi ya
ujenzi na ukarabati wa bandari hizo, ili kuboresha na kuhakikisha zinakuwa imara zaidi
kwa kupokea mzigo ya kutosha.
“katika kutekeleza na kuhakikisha
kuwa sekta hii inaimarika azma kubwa tuliyonayo sisi kama Sekritarieti ya Miundombinu
ni kuboresha na kuhuisha sekta hii ili iweze kufanyakazi kwa ufanisi na uhakika zaidi. Sekritarieti inaendelea na mpango mkakati
wa mwaka 2012-2021 na kuungwa mkono na Jumuiya ya Ulaya-EU ambao wako tayari kusaidia kuimarisha miundombinu katika nchi wanachama
wa SADC”, Amesema Makoena.
Katika Mpango mkakati huo Sekritarieti
ya Miundombinu inalenga zaidi katika kuimarisha na kuweka kanuni tisa (9) za pamoja kwa wanachama ikiwemo Udhibiti
wa Uendeshaji wa magari ya mizigo barabarani, viwango na vipimo vya magari ya
mizigo na mizani ya kupima magari yote, kwani kanuni hizo ni muhimu kwa usalama wa
barabara na bidhaa.
Pia, Machi mwaka 2018 SADC
ialisaini makubaliano ya Sheria ya usafirishaji wa kuvuka mipaka miongoni mwa nchi wanachama inayojulikana kama Cross-Border Road Transporter-Regulator
Forum (CBRT-RF). Ambayo inafanyakazi pamoja na Transport and Transit Facilitation Program (TTFP) yenye kazi ya
kusimamia mambo ya usafirishaji yote hayo ni kuhakikisha Sekta ya usafirishaji inakuwa imara katika Jumuiya hiyo.
Makoena aliongeza na kusema kuwa
sekta ya usafirishaji kwa upande wa Anga inaimarishwa ili kuwezesha kuwepo na ndege kubwa za mizigo katika ukanda huo
wa kusini mwa afrika. Kwani usafiri wa anga ni moja ya kichocheo muhimu katika kutekeleza ujenzi
wa viwanda.
Hivyo, Sekritarieti
ya Miundombinu inatekeleza hilo kwa kuanzisha Taasisi ya masuala ya usalama wa
usafiri wa Anga (SADC Aviation Safety
Organization, SASO) inayoshughulikia masuala ya usafiri wa
anga katika nchi wanachama wa Jumuiya hiyo.
Pamoja na hayo, SADC
miundombinu inaendelea na utekelezaji wa ukarabati na ujenzi wa
Reli katika Nchi wanachama ili kuimarisha na kulinda usalama wa barabara, kwani mizigo mizito itakuwa inasafarishwa
kwa njia ya treni na kuepuka uharibu wa barabara.
Akimalizia Makoena alisema
kuwa katika sekta ya Nishati SADC inajivunia utekelezwaji wa Mradi Mkubwa wa
Ujenzi wa Bwawa la Umeme la Mto Rufiji nchini Tanzania, ambapo wanachama wa
SADC watafaidika na umeme huo.
“Tunajivunia mradi huu,
siyo SADC Jumuiya ya Afrika Mashariki-EAC, na tunakubaliana na kumuunga mkono
kwa uongozi na mafanikio makubwa kwa Rais wa Sasa wa Tanzania katika utekelezaji wa
mradi huo, tunahitaji kufanikisha hili kwa sababu tunahitaji Miundo mbinu hii. Amesema Makoena
No comments:
Post a Comment