Naibu wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,Mhe. Juliana
Shonza akijibu swali wakati wa kikao cha tatu cha Mkutano wa 16 wa Bunge leo
tarehe 5 Septemba 2019 jijini Dodoma.
Na. Shamimu Nyaki –WHUSM
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo Mhe.Juliana Shonza amesema kuwa Serikali haishikizi ufadhili katika
michezo bali wajibu wake ni kuweka mazingira wezeshi kwa mfadhili ambaye
anataka kufadhili mchezo wowote kutokana na yeye kuona namna anavyoweza
kufaidika katika ufadhili huo.
Mhe.Shonza amesema hayo leo Bungeni
Dodoma alipokuwa anajibu swali la Mbunge Mhe.Sophia Mwakagenda (Viti Maalum)
aliyeuliza Ni lini Serikali itahakikisha ufadhili unapatikana kwenye michezo
inayohusu wanawake hususan michezo ya ngumi.
Akijibu swali hilo Mhe.Shonza ameeleza
kuwa ufadhili wa michezo hutokana na mfadhili kuona faida ya kibiashara na
kijamii wakati anapofadhili ambapo amesititiza kuwa hivi sasa Tanzania ina ligi
kuu ya mpira wa miguu kwa wanawake ambayo inadhaminiwa na Kampuni ya vinywaji
ya Serengeti Breweries kupitia bia yake ya Serengeti Lite ambayo imefadhili
kutokana na faida walioona itapata.
“Ufadhili haushinikizwi na Serikali
bali ni suala la hiari kwa upande wa wafadhili ambao huchukua fursa hiyo pale
wamapoona fursa za kibiashara zitakazowanufaisha wao, Hivyo wajibu wa Serikali
ni kuimarisha uhusiano na kuweka mazingira wezeshi ili faida ipatikane kwa
pande zote mbili”alisisitiza Mhe.Shonza.
Aidha Mhe. Shonza katika kujibu swali
la nyongeza la mbunge huyo aliyeuliza ni lini Serikali itatoa vifa vya mazoezi
kwa wanamichezo hao, ameeleza kuwa suala la kukuza na kuendeleza michezo nchini
linashirikisha pia wadau hivyo ni wajibu wa wanachi wote kuona michezo kuwa ni
muhimu katika jamii hivyo kuwekeza katika Nyanja mbalimbali.
Hata hivyo Mhe. Shonza amewaomba wadau
wote wa Michezo nchini kusaidia kushawishi makampuni,Taasisi na wadau wote
kudhamini na kufadhili maendeleo ya michezo nchini ikwemo wanayoshiriki
wanawake.
No comments:
Post a Comment