Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Shein Awaapisha Viongozi Aliowateua Hivi Karibuni.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimuapisha Bw.Abdalla Rashid Abdulla  kuwa Mshauri wa Rais Mambo ya Siasa Zanzibar hafla hiyo imefanyika leo katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akimkabidhi hati ya kiapo  Bw.Ali Mzee Ali baada ya kumuapisha kuwa mshauri wa Rais katika masuala ya Historia na Mambo ya Kale Zanzibar , hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Ikulu Kjijini Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewapisha Washauri wa Rais wa Zanzibar na  Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliowateua hivi karibuni.

Walioapishwa ni Bwana Abdalla Rashid Abdalla aliyeapishwa kuwa Mshauri wa Rais Mambo ya Siasa.

Aidha, Dk. Shein amemuapisha Bwana Ali Mzee Ali kuwa Mshauri wa Rais katika Masuala ya Historia na Mambo ya Kale.

Hafla ya kuwapishwa viongozi hao ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akiwemo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Idd, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid

Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu, Mawaziri, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Said Hassan Said, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee na Makatibu Wakuu. 

Wengine ni Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih, Naibu Kadhi wa Zanzibar Sheikh  Hassan Othman Ngwali, Mkuu wa  Mkoa wa Mjini Magharibi Hassan Khatib Hassan, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib, Viongozi wa Vikosi vya SMZ, Washauri wa Rais wa Zanzibar, viongozi wengine wa Serikali pamoja na wanafamilia.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.