Habari za Punde

Viongozi wa Idara za Serikali Kutumia Vema Dhamana Zao.

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Nd. Abdullah Hassan Mitawi akishauri umuhimu wa Wataalamu wa Mamlaka ya kuzuia na kuhujumu uchumi kutumia Lugha ya alama katika kutoa elimu kwa Watu wenye Mahitaji Maalum.
Na.Ali Mtwama.OMPR.
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu  wa  pili wa Rais Zanzibar Ndugu  Shaaban Seif  Mohamed  amesema  Ofisi  ya Makamu wa pili wa Rais  itaendelea kutoa huduma bora  kwa wananchi kama inavyoelekezwa kisheria ili kuepukana na mwanya  wa upokeaji Rushwa na uhujumu  uchumu kwa watumishi wa Umma.
Amesema kuwa   viongozi wa Idara na Taasisi mbali mbali za Serikali  wana haki na wajibu wa kuendesha  na kutumia vyema  dhamana walizopewa   pamoja na kusimamia  wafanyakazi wao kufuata sheria  na taratibu za kazi  ili kuweza kutoa huduma bora  kwa Umma.
Nd.Shaaban Seif Mohamed amesema hayo wakati akifungua mafunzo  mafupi ya kupambana na Rushwa yaliyoshirikisha Wakurugenzi wa Idara na Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya makamu wa pili  mafunzo yaliyoandaliwa na maamlaka ya kuzuia na  Uhujumu uchumi Zanzibar {ZAECA ) ofisini kwake vuga  mjini Zanzibar.
Aidha amesema Ofisi ya Makamu wa Pili  kupitia Mtendaji Mkuu wa Serikali ambaye ndiye mwenyekiti wa kamati ya kupambana na  kuzuia Rushwa na  hujumu Uchumi Zanzibar   itahakikisha inapambana  dhidi ya uhujumu uchumi  pamoja na kutoa mafunzo  kwa watendaji  wake.
Alisema Mafunzo hayo yatakuwa yakisimamiwa na wataalamu  kutoka ofisi ya   Utumishi na Utawala  Bora  kupitia mamlaka ya Rushwa na uhujumu  Uchumi  Zanzibar  ili kuhakikisha Mapambano dhidi ya Rushwa  katika Utumishi wa Umma yanaimarika.
Alifahamisha kwamba katika mwaka wa Fedha 2019/20 Ofisi hiyo imetenga    bajeti zaidi kwa lengo za kuongeza kasi ya  kupambana  na Rushwa na uhujumu uchumi.
Kwa upande wake  Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya Kuzuia Rushwa  na uhujumu uchumi Ndugu Mussa  Haji Ali amesema ipo haja kwa Taasisi za kiserikali kushirikiana katika mapambano ya  Rushwa na uhujumu uchumi  ili Zanzibar  inafikia lengo  la kuondokana na tatizo la Rushwa  na Uhujumu uchumi  hasa katika Taassisi za Umma
“Kila moja wetu kupitia nafasi yake ya Utumishi wa Umma anahaki ya kusimamia wafanyakazi  wake  ili wanachokihudumia kinakuwa katika msingi ya maadili  ya utumishi wa umma  kwa kuzuwia mianya ya uhujumu uchumi”. Alisema  Mkurugenzi Mussa.
Akizungumzia suala la  fomu za maadili kwa viongozi wa Umma amesema kuwa kila mtumishi wa umma hasa Kiongozi ana dhamaan ya ujazaji wa fomu hizo ili kubainisha  kiwango cha mali anacho  miliki  kwa mustakabala wa kuepusha viashiria vya   Utowaji  Rushwa na uhujumu Uchumi.
Nao washiriki wa mafunzo hayo  wameitaka  mamlaka ya  kuzuia Rushwa na uhujumu uchumi kutowafumbia macho wale wote wanaofanya vitendo vya uhujumu uchumi   kwani kufanya hivyo kunachangia kuzoroteshwa maendeleo yanayokusudiwa kuwafikia wananchi.
 Kwa upande wake Naibu katibu mkuu Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar  Ndugu Abdulla  Hassan  Mitawi  ameishukuru  mamlaka ya kupambana na rushwa na uhujumu uchumi kwa kuwapatia  elimu hiyo  watendaji wa Ofisi hiyo na kuahidi kufanya nao kazi pamoja katika nyanya mbalimbali  ili kufikia lengo husika.
Nd. Mitawi aliushauri Uongozi na Watendaji wa Mamlaka hiyo kuwatumia wataalamu wa lugha za Alama watakaowasaidia  Wananchi wenye mahitaji maalumu ili nao wapate haki hiyo ya elimu ya Mapambano dhidi  ya Uhujumu uchumi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.