SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi kupanua wigo wa ushirikiano kati yake na Taasisi ya ‘China National Reseach Institute of Food & Fermentation Industries’ katika suala la upatikanaji wa mafunzo kwa watendaji wake kupitia sekta tofauti.
Ahadi
hiyo imetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum, wakati alipozungumza na Mkurugenzi Mkuu
wa Taasisi hiyo Dong Jianhui Ofisini kwake.
Wakufunzi
kutoka taasisi ya ‘China National Reseach Institute of Food & Fermentation
Industries’ wapo nchini wakiendelea na utoaji wa mafunzo ya ya Upishi na
Ukarimu kwa watendaji wanaotowa huduma kwa Viongozi wakuu wa Serikali pamoja na
sekta binafsi, mafunzo yaliodumu kwa takriban wiki tatu na kutarajiwa kumalizika
Oktoba 08, mwaka huu.
Alisema
Serikali itaendeleza ushirikiano kwa kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na
uongozi wa taasisi hiyo katika utoaji wa mafunzo ya Upishi na ukarimu kwa mwaka wa tatu hivi sasa, pamoja na
kaungalia uwezekano wa kuyafikia maeneo mengine.
Alisema
ushirikiano huo utaimarika kikamilifu pale Serikali itakapofanikisha hatua za
kutuliana saini makubaliano ya awali (memorandum of understanding) kati yake na
taasisi hiyo.
Aidha,
aliipongeza Wizara inayosimamia upatikanaji wa mafunzo ya nchini China kwa
kuunga mkono utoaji wa mafunzo hayo kwa mwaka wa tatu mfululizo, hivyo kuleta mabadiliko makubwa na kuinua uwezo wa watendaji nchini.
Salum,
alieleza matumzini yake ya kiongozi huyo
kukutana na viongozi wa Idara ya Maendeleo ya Utalii, iliyo chini ya
Chuo Kikuu cha Taifa SUZA pamoja na Wakala wa Chakula, dawa na Vipodozi ili
kuweza kubadilishana uzoefu na utaalamu katika kipindi atakachokuwepo nchini.
Nae,
Mkurugenzi Mkuu kutoka taasisi ya ‘China
National Reseach Insitute of Food & Fermentation Industries’ Dong Jianhui
alisema taasisi hiyo itaendelea kutoa mafunzo ya upishi na ukarimu kwa
watendaji mbalimbali, ikiwa ni hatua ya kuendeleza uhusiano na ushirikiano kati
yake na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Aliipongeza
Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa juhudi zake na kuunga
mkono na kufanikisha utoaji wa mafunzo hayo.
Aidha,
Mkurugenzi huyo alisifia mandhari nzuri ya Zanzibar pamoja na usalama wa
kutosha uliopo hapa nchini.
Katika
hatua nyengine, kiongozi huyo alikutana na Uongozi wa Chuo Kikuu cha Taifa (SUZA) na Wakala
wa Chakula, Dawa an Vipodozi na kuahidi kuendeleza uhusiano na ushirikiano kati
ya taasisi hizo kwa mustakbali mwema na maendeleo ya Zanzibar.
Dong
alisema katika maeneo mbali mbali aliyotembelea ikiwemo la uzalishaji wa viungo
Kizimbani, amebaini Zanzibar kuwa na
utajiri mkubwa bidhaa za chakula, lakini
kilichokosekana ni utaalamu wa kusarifu bidhaa hizo, hivyo alibainisha azma ya
Taasisi hiyo kusaidia utaalamu ili kuziongea thamani bidhaa hizo na kuleta tija
katika soko la Utalii.
Aidha
Mkurugenzi huyo alitembelea Ofisi za Wakala wa Chakula, Dawa na Vipodozi
zilizopo Mombasa na kukutana na uongozi wa Wakala huo, ambapo uongozi wa
taaasisi hiyo umeomba msaada wa kuwajengea uwezo watendaji wake kwa kuwapatia
mafunzo ili waweze kutekeleza vyema majukumu yao.
Mkurigenzi
Mtendaji wa Wakala wa Chakula, Dawa na Vipodozi Dk. Burhan Othman alisema kuna
umuhimu kwa watendaji wa Ofisi kupatiwa fursa za mafunzo yatakayowajengea
uwezo, hususan katika suala la ukaguzi wa chakula.
Nae, Mkurugenzi
Taasisi ya Utalii Zanzibar, iliyo chini ya Chuo Kikuu cha Taifa SUZA, Dk. Aley Soud aliiomba taasisi hiyo
kuzingatia mahitaji yaliopo kwa kubadilishana na uzoefu na fursa za mafunzo kwa
watendaji wa taasisi hiyo, ikiwa ni hatua ya kuongeza ushirikiano kati ya
taasisi hizo mbili.
Alisema
wakati huu Zanzibar ikiimarisha uchumi wake kupitia sekta ya utalii kumekuwepo
na ongezeko kubwa la Watalii kutoka China wanaozuru nchini.
Abdi
Shamna, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777476982. Fax: 024 2231822
E-mail: abdya062@gmail.com
No comments:
Post a Comment