Afisa
Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Mwalim Moh’d Nassor Salim
akizungumza na walimu wa Skuli mbali mbali za Sekondari walioajiriwa mwezi
Oktoba 2018 na mwezi Mei 2019
Afisa
Mdhamini Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Massoud Ali Mohamed akizungumza na walimu wa Skuli mbali mbali za
Sekondari walioajiriwa mwezi Oktoba 2018 na mwezi Mei 2019 katika Ukumbi wa
Skuli ya Maandalizi Madungu Chake Chake Pemba.
Walimu
wa Skuli mbali mbali za Sekondari kisiwani Pemba walioajiriwa mwezi Oktoba 2018
na mwezi Mei 2019 wakiwa katika Ukumbi wa Skuli ya Maandalizi Madungu Chake
Chake Pemba.
Na Ali Othman, Pemba
WALIMU
kisiwani Pemba wametakiwa kufanya kazi kwa weledi na nidhamu katika utekelezaji
wa majukumu yao ya kila siku wanapokua katika mazingira ya kazi.
Wito
huo umetolewa na Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba,
Mwalim, Mohamed Nassor Salim katika semina elekezi kwa walimu wapya iliyofanyika katika ukumbi wa Skuli ya
Maandalizi Madungu Chake Chake Pemba.
Mwalimu
Moh’d amwataka walimu hao kuwa mfano nzuri wa kuigwa katika nidhamu na uwajibikaji
ili waweke kumbukumbu ya huduma njema kwa jamii.
Aidha
aliwataka walimu hao kukemea vitendo vya udhalilishaji pamoja na kutojihusisha
katika mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi kwani kufanya hivyo ni kwenda
kinyume na misingi ya ualimu na kanuni za utumishi wa umma.
“Walimu
ni kioo cha jamii hivyo mnapaswa kufanya kazi kwa umakini mkubwa” alisema
Mwalimu Moh’d
Akiendelea
kutoa nasaha zake kwa walimu haoAfisa Mdhamini pia amewataka walimu hao kuwa na utamaduni wa
kujisomea na kujiandaa vizuri kwa masomo wanayofundisha ili kuepusha
sintofahamu na wanafunzi wao.
Kwa
upande mwengine Mwalimu Moh’d amewaasa walimu hao kutojihusiha na masuala ya
kisiasa badala yake wajikite kufundisha ili kuendelea kuinua kiwango cha ufaulu
nchini ambacho kimekua kikipanda kila mwaka.
Ameeleza
kuwa walimu hawana budi kutambua kuwa wapo kwa ajili ya kutoa elimu kwa watoto
hivyo wanapaswa kutambua jukumu na wajibu huo.
Amebainisha
kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya uongozi wa Dk. Ali Mohamed
Shein, imekua ikichukua juhudi za makusudi katika kuboresha sekta ya elimu
nchini ikiwemo ujenzi wa skuli za kisasa kila wilaya Unguja na Pemba pamoja na
kutoa scholarship kwa wanafunzi wanaofaulu vizuri katika mitihani yao ya kidato
cha sita.
Naye,
Afisa Mdhamini Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Massoud Ali
Mohamed amewashauri walimu hao kutobadilisha fani zao wanapojiendeleza
kitaaluma kwani kufanya hivyo kunapekelekea tatizo la uhaba wa walimu.
Katika
hatua nyengine , Bwana Massoud amewasihi
walimu hao kutumia nafasi walizonazo katika kukemea vitendo vya rushwa na
udhalilishaji ambavyo vimekithiri katika jamii.
Aidha
amewataka walimu hao kuwa na moyo wa uzalendo na kuipenda nchi yao pamoja na
kuthamini juhudi mbalimbali za serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi
wake ikiwemo kuboresha sekta hiyo ya elimu.
Mafunzo
hayo elekezi ya siku mbili kwa walimu wapya yameandaliwa na Wizara ya Elmu na
Mafunzo ya Amali Pemba yakishirikisha walimu wapya 101 kutoka Skuli mbali mbali
za Sekondari kisiwani Pemba.
No comments:
Post a Comment