Habari za Punde

Mahafali ya 33 ya Chuo Cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akimtunuku Shahada ya Mipango na Usimamizi wa Mazingira mmoja wa wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, katika Mahafali ya 33 ya chuo hicho ambapo aliwasihi wahitimu hao kutumia elimu waliyoipata kujiajiri.
Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma wakivaa kofia baada ya kutunukiwa Astashahada na Shahada mbalimbali katika Mahafali ya 33 ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere chuoni hapo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akizungumza na Wahitimu na watumishi wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, katika mahafali ya 33 ya Chuo hicho ambapo aliuagiza uongozi wa chuo hicho kuongeza juhudi katika masuala ya tafiti zinazolenga kutatua changamoto mbalimbali za maendeleo na kupunguza umaskini.
Kamishina Msaidizi wa Bajeti kutoka Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Pius Mponzi, akitoa neno la kumkaribisha mgeni rasmi wa mahafali ya 33 Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani), kwa niaba ya Katibu Mkuu waWizara hiyo.
Mkuu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini, Prof. Hozen Mayaya akitoa hotuba katika Mahafali ya 33 Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya  Dodoma.
Baadhi ya Wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (hayupo pichani) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika Mahafali ya 33 ya chuo hicho.
Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma wakivaa kofia baada ya kutunukiwa Astashahada na Shahada mbalimbali katika Mahafali ya 33 ya chuo hicho yaliyofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere chuoni hapo.
Jumuiya ya Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini Kampasi Kuu ya Dodoma, wakimsikiliza Mkuu wa Chuo hicho Prof. Hozen Mayaya, akitoa hotuba wakati wa Mahafali ya 33 ya Chuo hicho ambapo wahitimu 3,182 wa,etunukiwa Astashahada na shahada mbalimbali.

(Picha na Farida Ramadhani-Wizara ya Fedha na Mipango)
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akipokea zawadi ya mipira kutoka kwa Mkuu wa Chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini, Prof. Hozen Mayaya katika Mahafali ya 33 ya Chuo hicho Kampasi Kuu ya Dodoma, mipira hiyo imetengenezwa katika kiwanda cha kujenga kiwanda cha kuchakata na kutengeneza bidhaa za ngozi katika kijiji cha Idifu Wilaya ya Chamwino, Mkoa wa Dodoma ambapo Chuo kimewekeza jumla ya shilingi milioni 396.
(Picha na Farida Ramadhani-Wizara ya Fedha na Mipango)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.