Mwenyekiti wa (THBUB), Jaji Mstaafu
Mathew Mwaimu akiongea na wafanyakazi wa tume pamoja na wageni wengine
waliohudhuria hafla fupi.
Na. Mbaraka Kambona,
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu
na Utawala Bora (THBUB), Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu ametembelea ofisi za
taasisi hiyo zilizopo visiwani Zanzibar, ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu alipokabidhiwa dhamana hiyo Novemba 4, 2019.
Jaji Mwaimu alifanya ziara hiyo mapema
leo (Novemba 30, 2019) kwa lengo la kutambuana na wafanyakazi wa tume waliopo
katika ofisi hizo zilizopo Mbweni, visiwani Zanzibar.
Katika ziara hiyo, Jaji Mwaimu
akiongozana na Makamishna na viongozi wengine wa tume alifanya ukaguzi wa ofisi
hizo ambazo hivi karibuni zilifanyiwa ukarabati mkubwa kwa lengo la
kuziboresha.
Akiongea baada ya kumaliza ukaguzi wa jengo
hilo, Jaji Mwaimu alieleza kuridhishwa kwake na ukarabati huo uliofanyika, na
kusema kuwa watajipanga vizuri katika majukumu yao ili kuhakikisha wanazitumia
vizuri ofisi zote mbili za Tanzania bara
na hizo za visiwani ili kutatua kero za wananchi.
Aidha, Jaji Mwaimu aliwashukuru Shirika
la Kimataifa la Maendeleo (UNDP) kwa ufadhili wao ambao umewezesha kufanikisha
ukarabati huo.
Katika
ziara hiyo Jaji Mwaimu aliambatana na viongozi wafuatao; Makamu Mwenyekiti,
Mohamed Khamis Hamad, Mheshimiwa, Dkt.
Fatma Rashid Khalfan, Mheshimiwa Thomas Masanja, Mheshimiwa Amina Talib Ali, Mheshimiwa Khatib
Mwinyi Chande na Mheshimiwa Nyanda
Josiah Shuli.
Jaji Mwaimu (kushoto) akiongea na
Kamishna Mkaazi wa tume visiwani Zanzibar, Khatib Mwinyichande wakati wakikagua
ofisi hizo za tume.
Afisa Mfawidhi wa tume Zanzibar, Hussein Mbarouk akimuonesha
kitu Mwenyekiti (wa kwanza kushoto) wakati wa ukaguzi wa jengo hilo.
Mwenyekiti wa (THBUB), Jaji Mstaafu
Mathew Mwaimu (aliyeinama) akiwaongoza viongozi wengine wa tume kuwatunza
waburudishaji wa kikundi cha ngoma ya kibati kutoka Zanzibar katika hiyo hafla
fupi.
No comments:
Post a Comment