Na. Lulu Mussa - Morogoro
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais
(Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Sima amesema Serikali imefanya mapitio ya
Kanuni ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira ili kurahisha uwekezaji nchi.
Akizungumza na Wafanyabiashara na Wawekezaji katika
Mkutano wa Mashauriano baina yao na Serikali katika ukumbi wa Hoteli
ya Glonency mkoani Morogoro, Naibu Waziri Sima amesema gharama za
kulipia vibali zimepungua na idadi ya siku
pia imepungua kutoka siku 145 mpaka siku 95 hivi sasa
“Ndugu zangu marekebisho haya yote yanayofanywa
na Serikali, yanalenga kurahisisha mchakato wa tathmini ya Athari kwa Mazingira
na kurahisisha uwekezaji hapa nchini, Mfano awali gharama kwa vituo vya mafuta
zilikuwa zaidi ya Milioni kumi na kwa sasa gharama hizi zimepungua hadi kufikia
Milioni Nne na nyingine Milioni mbili” Sima alisisitiza.
Katika hatua nyingine Naibu Waziri Sima,
amesema Ofisi yake inaandaa Kanuni za Wataalamu Elekezi wa Mazingira ili
kurahisisha uwekezaji kwa kuwa miradi yote ni lazima ipate cheti kutoka Baraza
la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC). “Tangu tumefanya mapitio
ya Kanuni zetu, malalamiko kutoka kwa wawekezaji yamepungua kwa kiasi kikubwa
sana” Sima alisisitiza.
Hata hivyo Naibu Waziri Sima amewakumbusha
washiriki wa Kikao hicho kuwa Mabadiliko ya tabianchi ni tatizo kubwa duniani,
na kutoa rai kwa umma wa watanzania kupanda miti kwa wingi
kupunguza athari za mabadiliko ya Tabianchi. Amewaagiza wawekezaji hasa wenye
Viwanda kuhakikisha wanaanzisha vitalu vya miche katika maeneo yao na kusisitiza
kuwa ukaguzi wa masuala ya Mazingira katika maeneo yao utaanzia hapo.
Mkutano huu wa Mashauriano baina ya Serikali, Wafanyabiashara
na Wawekezaji umelenga kusikiliza na kutatua changamoto zao umefanyika
leo katika ukumbi wa Hoteli ya Glonency mkoani Morogoro
na kuendelea katika Mikoa ya Pwani na Dar es Salaam. Jumla ya Mawaziri na
Manaibu Waziri 13 wanashiriki Mkutano huu.
No comments:
Post a Comment