Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya
Michezo wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bw.Yusuph Singo akifafanua kuhusu usajili wa
wanamichezo wa kigeni hapa nchini leo Aprili 29,2020 Jijini Dodoma.
Na
Shamimu Nyaki, WHUSM-Dodoma
Serikali
haijatoa ukomo wa wachezaji kutoka nje kushiriki michezo hapa nchini bali
imeibua mjadala kwa wadau ili watoe maoni yao.
Hayo
yamesemwa leo Jijini Dodoma na Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo
Bw.Yusuph Singo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ikiwa ni
hatua ya kuboresha na kuimarisha sekta ya michezo nchini.
Ili
kutekeleza mjadala huo, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) limepewa jukumu la kuendelea
kuandaaa mwongozo utakaotumika kukusanya maoni kutoka kwa wadau kuhusu ukomo wa
wanamichezo wa nje hapa nchini.
“Katika
Hotuba ya Bajeti iliyosomwa hivi karibuni Bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe, hakuongolea idadi ya
wachezaji kutoka nje wanaotakiwa kucheza nchini, bali aliagiza BMT kuandaa
mjadala mpana katika kukusanya maoni kwa wadau wa michezo kuhusu namna bora ya
kusajili wachezaji wa kigeni katika michezo yote hapa nchini” alisema Bw. Singo.
Pamoja
na hayo, Mkurugenzi huyo ambainisha kuwa Mhe.Waziri Dkt. Mwakyembe alisisitiza
kuwa wanamichezo wote kutoka nje ya nchi wanaosajiliwa hapa nchini ni lazima
wawe na ubora pamoja na viwango vinavyotakiwa.
Akifafanua
suala hilo Bw. Singo amesema kuwa michezo yote ya kulipwa kwa sasa imeendelea
kukua duniani kote na nchi yetu pia inayo wachezaji wengi wanaocheza michezo hii
ikiwemo Mpira wa Kikapu (Basketball), Kriketi, Mpira wa Miguu na michezo
mingine, hivyo, Serikali haijatoa maelekezo ya ukomo wa usajili wa idadi ya
wachezaji bali inataka kuwepo kwa mjadala wa wazi utakaotoa mwongozo wa ukomo
wa idadi ya usajili wa wachezaji wa kigeni.
Aidha,
Mkurugenzi huyo alitoa rai kwa wadau wa michezo nchini watakapopata fursa ya kuchangia
au kutoa maoni katika mjadala huo wasiegemee katika timu wanazoshabikia, bali
watoe maoni ambayo yatasaidia kuendeleza michezo na kuendeleza vipaji vya
wanamichezo wetu pamoja na kukuza michezo nchini.
No comments:
Post a Comment