1. Kirusi hichi
hakina uhai lakini ni aina ya protini iliyozungukwa na utandu wa mafuta (lipid fats)
ambayo yakipenya kwenye tundu za macho, pua au mdomo hujibadilisha (mutation) na
hujizalisha kwa wingi na kuanza kushambulia seli za mwili na hasa mapafu.
2. Kwa kuwa kirusi chenyewe hakina uhai hakiwezi kuuliwa lakini huharibika wenyewe. Muda wa
kuharibika kwake hutegemea na joto, unyevu unyevu na sehemu kilipopatikana.
3. Kirusi ni
kitepetepe mno kwani kimehifadhiwa na utandu mdogo wa mafuta hivyo sabuni
yoyote ikitumika kunawia huondosha ule utandu ndiyo maana hutakiwa kuosha
mikono kwa kuisugua vizuri kwa uchache sekunde 20 na hapo kirusi
huharibika na kutokuwa na madhara tena.
4. Joto huyeyusha utandu wa mafuta yaliyokizunguka kirusi cha Corona hasa ukitumia maji yenye vuguvugu zaidi ya
nyuzi joto 25 kuoshea mikono au hata nguo na chochote chengine.
5. Aina yoyote ya
kilevi chenye zaidi ya asilimia 65, huyeyusha mafuta yoyote hasa ule utandu wa juu wa kirusi cha Corona.
6. Kirusi cha Corona
hakina uhai hivyo hakiwezi kutibika na Antibiotics. Antibiotics hutibu bakteria
viumbe walio hai.
Imetafsiriwa
kutoka John Hopkins University
No comments:
Post a Comment