Na Ali Shaaban \Juma
Muuguzi akiwa
mtoto wa Lina Medina aliyelala kitandani baada ya kujifungua akiwa na
umri wa miaka mitano hapo mwaka tarehe 14 Mei, 1939.
Katika
hali isiyo ya kawaida, msichana aitwae
Lina Medina ameweka kumbukumbu duniani kwa kuwa mwanamke mwenye umri mdogo
kabisa kubeba mimba na kujifungua.
Lina
Medina alizaliwa tarehe 13 Septemba,
1933 katika mji wa Ticrapo huko nchini Peru. Baba yake mzazi ni muhunzi
aliyeitwa Tiburelo Medina na mama yake ni Victoria Losea.
Akiwa
na umri wa miaka mitano, binti huyo aliumwa na ndipo wazazi wake walipoamua
kumpeleka hospitali wakilalamika kuwa mtoto wao huyo amekuwa akisumbuliwa na
tumbo kwa muda mrefu. Kama ilivyo kawaida, baada ya kufikishwa katika hospitali
ya mji wa Pisco na kufanyiwa uchunguzi wa kitaalamu, madaktari wa hospitali
hiyo walipigwa na mshangano pale walipogundua kuwa msichana huyo wa miaka
mitano alikuwa na mimba ya miezi saba.
Daktari
aitwae Geraldo Lozada wa hospitali hiyo ndiye aliyepewa jukumu la kumsimamia
binti huyo. Kutokana na kuwa binti huyo alikuwa na mimba akiwa na umri mdogo,
Dakatari Lozada alishauri msichana huyo apelekwe katika hospitali kuu ya nchini
Peru iliyoko katika mji mkuu wa nchi hiyo Lima. Baada ya kufikishwa katika
hospitali kuu ya mjini Lima na kufanyiwa
uchunguzi zaidi wa kitaalamu, madaktari waligundua kuwa binti huyo alizaliwa na
hali isiyo ya kawaida ya kukuwa kwa viungo vya uzazi katika umri mdogo ambayo
kitaalamu inajulikana kama “precocious
puberty”.
Kwa ufupi hali ya “precocious puberty” humfanya msichana kuvunja ungo
mapema na kupata mzunguko wa damu ya hedhi katika umri mdogo kulika hali ya
kawaida. Kitaalamu katika hali ya kawaida msichana, huvunja ungo akiwa na
wastani wa kati ya miaka 10 hadi 11.
Uchunguzi ulofanywa na madaktari kwa binti huyo ulibaini kuwa alivunja
ungo na kupata mzunguko wa damu ya hedhi akiwa na umri wa miaka miwili na nusu
au mitatu na alichuchua maziwa akiwa na miaka minne.
Akiwa na miaka mitano, tayari viungo vya uzazi vya binti huyo vilikuwa
tayari kupokea na kulea mimba.
Lina Medina na mwanawe wa kiume aitwae Gerardo
ambae alipokuwa mdogo alidhani kuwa mama
huyo ni dada yake.
Lina Medina alijifungua tarehe 14 Mei, 1939 akiwa na umri wa miaka mitano, miezi saba na
siku 21 akiwa ndiye mwanamke aliyeweka historia duniani kuzaa akiwa na umri
mdogo. Alijifungua kwa operesheni maalum iliyofanywa na madaktari watatu ambao
ni Dakatari Lozada akishirikiana na
Busalleu na Daktari Colareta. Mtoto huyo wa kiume alikuwa na uzito wa ratili 6
(Gramu 2,700) na alipewa jina la Geraldo la mkunga aliyemzalisha mama
yake. Binti huyo alitoka hospitali na
mwanawe wakiwa na afya nzuri baada ya siku
chache.
Kwa vile tukio hilo si la kawaida, kulijengeka dhana katika jamii ya
taifa la Peru kuwa binti huyo alibakwa na kupata mimba hiyo. Awali, polisi
walimkamata baba mzazi wa mtoto huyo kwa tuhuma za kumbaka binti yake, lakini
baadae aliachiwa kwa kukosekana ushahidi.
Licha ya juhudi kubwa zilizofanywa na watu kadhaa kutaka binti huyo
amtaje aliyempachika mimba hiyo, Lina Medina hakumtaja aliyempa uja uzito huo.
Hata hivyo kwa mujibu wa mapitio ya kesi hiyo yalofanywa mwaka 1955, ilionekana
kuwa makabila mengi ya wahindi wekundu wanaoishi sehemu za vijijini huko nchini
Peru na Marekani ya kusini kwa ujumla yana sherehe nyingi za jadi ambazo
hatimae hutoa fursa ya ubakaji wa
wasichana na wanawake na hatimae kusababisha uja uzito usiotarajiwa.
Geraldo alikuwa akiamini kuwa Lina Medina ni dada yake na alijua kuwa
huyo ni mama yake alipofika umri wa miaka kumi ambapo katika mwaka 1979, kijana
huyo alijihusisha na harakati za afya ya uzazi katika jamii hadi alipofariki
dunia kutokana na maradhi ya mifupa akiwa na miaka 40.
Lina Medina aliajiriwa kama katibu muhutasi katika hospitali binafsi ya
Dokta Lozada huko mjini Lima, ambapo pia Daktari huyo alimsaidia binti huyo
kujiendeleza kielimu pamoja na mtoto wake. Baadae katika mwaka 1972, Lina Media
aliolewa na Raul Jurado ambapo walikuwa wakiishi katika mtaa uitwao Chicago Chico mjini
Lima. Alijifungua mtoto wake wa
pili miaka 33 baada ya kuzaa mtoto wake
wa kwanza alipokuwa na miaka mitano.
Mara kadhaa binti huyo alifuatwa na vyombo mbalimbali vya habari
yakiwemo magazeti, Televisheni na Redio maarufu za Marekani na Canada kwa ajili
ya kufanywiwa mahojiano ambapo alikataa.
Kwa mara ya mwisho, Lina Medina alifuatwa na wandishi wa habari wa
Shirika la Habari la Uingereza “Reuters” hapo mwaka 2002 kwa ajili ya mahojiano
ambapo pia alikataa.
Katika miaka ya hivi karibuni, nyumba
anayoishi na mumewe imevunjwa kwa ajili ya utanuzi wa barabara ambapo
amelalamikia kulipwa fidia ndogo ya
nyumba yao ambapo pia fidia iliyoahidiwa
na serikali kutokana na kujifungua akiwa
na umri mdogo hakupewa hadi leo.
Soma makala hii na nyenginezo katika Blog ya Rafikifumba.com
Sijakubaliana na hilo
ReplyDelete