JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
Mji wa Serikali Mtumba,
Mtaa wa Habari,
P.O.
Box 25,
40481 DODOMA.
|
TAARIFA KWA UMMA
UJUMBE WA SIKU YA
UANUWAI WA UTAMADUNI DUNIANI
21 MEI, 2020, Dodoma
Tanzania inaungana na dunia nzima katika kuadhimisha
sherehe ya Uanuwai wa Utamaduni ambazo hufanyika kila mwaka tarehe 21 Mei.
Katika sherehe za mwaka huu wa 2020, kila mwanajamii kwa nafasi yake na katika
eneo lake aendelee kuchukua tahadhali zinazoendelea kutolewa na Serikali juu ya
kupambana na janga hili la ugonjwa wa Covid 19 nchini na kuendelea na shughuli
za kiuchumi.
Tunajivunia na kuuenzi Uanuwai wa Utamaduni nchini kwa zaidi ya miaka 56 ya
Uhuru ambapo uanuai wa Utamaduni wa jamii zaidi ya 120 umekuwa fursa ya kuleta
amani, faraja, usawa na maendeleo kwa jamii ya Watanzania. Nina thubutu kusema
Uanuwai wa Utamaduni ni sawa na mishipa ya damu kwenye mwili wa binadamu.
Uanuwai wa utamaduni umeendelea kuwa ngao na kinga ya jamii dhidi ya
majanga mbalimbali yanayolikumba Taifa na Dunia. Uanuwai huu, umejipambanua
katika mila na desturi, sanaa, lugha na historia za jamii ya Tanzania.
Kila
mwanajamii amewajibika katika kutoa mchango wa maendeleo ya uanuwai wa
utamaduni iwe kwa kuheshimu utamaduni wake kufanya kazi kwa bidii, kutunza
amani ya nchi, kuheshimu vitambulisho na rasilimali za Taifa, sheria na
taratibu zote zilizowekwa na Nchi.
Kutokana na juhudi hizi, Watanzania wamekuwa mstari wa mbele katika
kulinda, kuendeleza na kuhifadhi anuwai wa kiutamaduni nchini hatua ambayo
imeleta urahisi wa kukabiliana na janga la dunia la ugonjwa wa homa kali ya
mapafu (COVID-19) kudhibitiwa
kikamilifu.
Viongozi wa Kitaifa, wasanii, wazee wa kimila na wazazi wametumia
majukwaa mbalimbali kujadili na kuelimisha umma umuhimu wa kujikinga na
kuwakinga wengine dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19.
Natoa wito kwa Watanzania wote kutunza na kuendeleza Uanuwai wetu wa Utamaduni,
kwani ukipotea hauna mbadala wake, tuzingatie kaulimbiu ya mwaka huu 2020
inayosema “Tulinde na Kudumisha Uanuwai
wa Utamaduni Wetu, Kwa Kufanya Kazi kwa Bidii na Kuchukua Tahadhali dhidi ya
Janga la Ugonjwa wa COVID-19”.
Kwa niaba ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nawatakia
maadhimisho mema.
Dkt. Harrison George Mwakyembe (Mb),
WAZIRI WA HABARI,
UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
No comments:
Post a Comment