Askofu Michael
Msonganzila Jimbo Katoliki Musoma
akiongoza ibada ya kumshuruku mungu kwa kulisaidia taifa kutokupata vifo vingi
vya kutokana na virusi vya Corona kama ilivyotabiriwa
na mataifa ya nje katika Parokia ya Shirati, ambapo alisisitiza watanzania kuendelea
kumuombea Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli
ili azidi kukua na kuongezeka imani na busara katika kuliongoza taifa, jana
Wilayani Shirati,Mkoani Mara.
Na Anitha Jonas – WHUSM,Shirati 01/06/2020
Watanzania tuendelea kumwombea Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli ili aendelee kukua na kuongezeka imani na
busara.
Askofu Michael Msonganzila wa Jimbo Katoliki Musoma
ametoa wito huo hivi karibuni katika ibada maalum ya kumshukuru mungu
iliyofanyika katika Parokia ya Shirati kwa ajili ya kumshukuru mungu kwa
kulisaidia taifa dhidi ya maambukizi ya Virusi vya Corona tofauti na
ilivyotabiriwa na mataifa ya nje nah ii ni kufutia maono Mheshimiwa Rais
yaliyosaidia taifa kukabiliana na janga la maambukizi ya Virusi vya Corona.
"Kwanini tung'ang'ane kupata taarifa za
idadi za vifo, taarifa hizi hazisaidii sana bali zinaongeza hofu tu
na pia hata taarifa za kweli zinapotolewa baadhi ya watu wanabeza kwa
Musoma hii mpaka sasa tunakifo kimoja tu cha mgonjwa wa Corona hakuna taarifa
zinazofichwa Kanisa Katolikili lina mfumo wa kupata taarifa kuanzia ngazi ya
familia na tunafuatilia ," alisema Askofu Msonganzila.
Pamoja na hayo askofu huyo alieleza
kuwa anafahamu katika kumshukuru mungu makundi mbalimbali ya imani tofauti
yalifanya maombi yao na katika Wilaya ya Shirati anafahamu kuwa wapo wazee wa
kijadi katika eneo hilo nao walifanya tambiko.
Halikadhalika nae askofu huyo
aliendeleea kusisitiza kuwa pamoja na idadi ya maambukizi kupungua lakini
ni vyema wananchi wanaendelea kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya wa kunawa
mikono kwa maji tiririka na sabuni, kuvaa barakoa na kuepuka msongamano.
Kwa upande wa Chifu wa Rorya Ngoje
Ogati alisema kuwa tangu janga hilo la virusi vya Corona lilipotangazwa wazee
wa eneo hilo kutoka koo mbalimbali walifanya
tambiko la kuzuia ugonjwa huo usifike katika eneo lao na mpaka sasa hakuna mtu
hata mmoja katika eneo hilo amepata virusi hivyo.
"Katika ibada yetu ya tambiko
tuliyofanya hivi karibuni nilakuzuia maambukizi ya virusi vya Corona katika
nchi yote kwa ujumla pamoja na kushukuru kwa eneo la Rorya kutokupata
maambukizi kabisa "alisema Chifu Ogati.
Nae Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo
ya Utamaduni Dkt.Emmanuel Temu alishukuru uongozi wa Wilaya ya Rorya kwa kuruhusu
makundi yote ya kiimani ikiwemo la wazee wa jadi kufanya ibada ya kushukuru na
kuliombea taifa.
Halikadhalika nae mmoja wa wakazi wa
Wilaya ya Rorya kutoka Kijiji cha Buturi Bi. Hudo Odemba alisema katika eneo
lao hawajawahi kupata maambukizi ya virusi vya Corona na anaamini kuwa
matambiko yaliyofanywa na wazee wa eneo hilo yamesaidia kuwakinga pamoja na
taadhari wanazochukua za kunawa mikono kwa maji tiririka kila mara.
Baadhi ya waumini wa
Kanisa Katoliki Parokia ya Shirati wakifuatilia ibada ya kumshukuru mungu kwa
kuliepusha taifa na maambukizi na vifo
vingi vya virusi vya Corona kama ilivyotabiriwa na mataifa ya nje
iliyokuwa ikiongoza na Askofu Michael Msonganzila Jimbo Katoliki Musoma (hayupo pichani) jana.
Baadhi ya viongozi wa
serikali ya wilaya ya Shirati na Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo wakiwa katika picha ya
pamoja na Askofu Michael Msonganzila
Jimbo Katoliki Musoma mara baada ya ibada ya kumshuruku mungu kwa
kulisaidia taifa kutokupata vifo vingi vya kutokana na virusi vya Corona kama ilivyotabiriwa na
mataifa ya nje, jana katika Parokia ya Shirati, mwenye tisheti ya mistari ni
Mkuu wa Wilaya ya Shirati Saimo Chacha,wa pili kushoto kwa waliyosimama mbele
ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Utamaduni Dkt. Emmanuel
Temu kuto Wizara ya Habari Utamaduni
Sanaa na Michezo.
Baadhi ya Wazee wa
Jadi Wilaya ya Rorya wakiwa katika picha
ya pamoja mara baada ya kufanya tambiko la kuliombea taifa dhidi ya janga la
virusi vya Corona wakiongozwa na Chifu wa eneo hilo Ngoje Ogati (watano kushoto) na mwenye tisheti ya mistari
ni Mkuu wa Wilaya ya Rorya Saimo Chacha na (watatu kulia ni) Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya
Utamaduni Dkt. Emmanuel Temu kuto Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo jana.
No comments:
Post a Comment