Timu ya Iringa all star veteran (IASV) ya mjini Iringa ikiwa imetoka katika mechi ya kila ya kujiandaa kwa ajili ya bonanza litakalofanyika jijini Dodom likaloshirikisha timu 24 kutoka mikoa 8 ya Tanzania Bara.
Na Fredy Mgunda,Iringa. Timu ya Iringa all star veteran (IASV) ya mjini Iringa
imejipanga vyema kuibuka kifedha katika bonanza litakalofanyika jijini Dodom
likaloshirikisha timu 24 kutoka mikoa 8 ya Tanzania Bara.
Akizungumza katika mazoezi ya mwisho yaliyofanyika katika
viwanja vya chuo cha Mkwawa nahodha wa timu hiyo Lissa Mwalupindu alisema kuwa
wachezaji wote wa timu hiyo wamefanya mazoezi na wapo timamu kuhakikisha
wanaibuka mabingwa kwenye bonanza hilo
Alisema kuwa timu hiyo inawachezaji wengi wazoefu na
wanauwezo mkubwa wa kucheza mpira na kupata ushindi kwenye bonanza hilo.
"Timu hii inawachezaji wengi waliocheza ligi kuu, ligi
daraja la kwanza, la pili na ngazi ya mkoa ambao wamefanya mazoezi kwa muda mrefu
na wamekubaliana kurudi na kombe hilo Mkoani Iringa, ili kutoa hamasa ya kwa
vijana kuwa na hari ya ushindani kupitia wao kama kioo"
Alisema kuwa bonanza hilo litakaloshirikisha timu kutoka
mikoa nane ambayo ni Pwani, Iringa, Dar es Salaam, Morogoro, Manyara, Arusha,
Kilimanjaro na wenyeji Dodoma.
Nao wachezaji wa timu
hiyo Davis Wapalila na Abissay Stesheni Jr walitoa onyo kwa timu binzani
kujipanga kwa kuwa timu hiyo ipo timu na inaenda kuchukua kombe na sio
kushiriki bonanza hilo.
"Sisi wachezaji tupo sawa kwelikweli na tumejipanga
kuhakikisha tunaibuka kuwa mabingwa wa bonanza hilo ambalo kwa mara ya kwanza
limezikutanisha timu nyingi kutoka mikoa
nane ya Tanzania Bara"walisema
Naye msemaji wa timu hiyo ya Iringa all star veterani Denis
Mlowe alitoa tahadhari kwa timu pinzani wajipange kwelikweli kwa kuwa timu ya
Iringa all stars veterani wanatimu ya ushindani na wamefanya mazoezi muda mrefu
na wamejipanga kushinda kombe hilo la bonanza hilo.
"Hawa wazee wako vyema kuhakikisha wanatoa dozi kwa
timu yoyote hivyo lengo ni kushinda bonanza hilo ambalo tumelichukulia umuhimu
mkubwa na kuwafundisha vijana jinsi ambavyo tulikuwa tunacheza zamani"
Alisema
Kwa upande wake Mratibu wa
timu hiyo ya Iringa all stars veterani Adv.Lupyana Massawa alisema kuwa
wachezaji wote wa timu hiyo watakuwepo kwenye bonanza hilo isipokuwa wachezaji
watatu waliopata majeruhi ambao ni Humphrey Ndale, Yohana Tembe na Petro Mrope
lakini wachezaji wengine wote wapo vizuri kabisa kwa ajili ya bonanza hilo
Aidha Massawa Aliongeza kuwa wachezaji watakaosafiri na timu
ni:
1. Attanas Maginga, 2. Adv. Evalisto Myovela, 3. Lissa Mwalupindi, 4. Tumaini Abbisai Stephen, 5. Pendo
Mapunda, 6. Abuu Silia, 7. Ally Ngalla,
8. Steve Lihawa, 9. Omary Daudi, 10.
Hasan Ussi, 11. Rashid Msigwa, 12. Ally Msigwa, 13. Dikson Kiboye, 14. Denis
Mlowe, 15.Khalid Fungabrek, 16.Pendo Mapunda,
17. Nicholaus Shari, 18.Petro Mrope, 19.Fredy Mgunda, 20.Davis Wapalila,
21.Ramadhani Shemhilu,22. Godlisten Mlaki,23.Ally Lwambano,24.Lusekelo Kibona, 25.Simba Yusuph
No comments:
Post a Comment