Habari za Punde

Zantel yatoa mafunzo kwa mawakala wake

Meneja wa Ezypesa Nuirat Zahor akiwafahamisha mawakala jinsi ya kutoa huduma kwa Wateja katika kongamano la mawakala lililofanyika jana Unguja-Zanzibar.Mawakala hao walihimizwa kuzingatia sheria na taratibu za utoaji wa huduma hiyo ili kuleta tija zaidi.

Mmoja wa mawakala wa Ezypesa Ramadhan Bilali Khalid akichangia hoja juu ya utoaji huduma ya umeme katika kongamano la kuwakumbusha mawakala kufata sharia za kazi zao huko holi la kiembe samaki karibu na sheli.  



·        Yahimiza kuzingatia sheria ili huduma hiyo iwe na tija kwa Taifa.

 

Zanzibar.

Kampuni ya simu za mkononi Zantel, imeendesha mafunzo kwa mawakala wake na kuwataka mawakala wa kampuni hiyo kuhakikisha wanafuata sheria na taratibu za nchi katika ufanyaji wa kazi zao ili waweze kuleta tija hapa nchini.

 

Wito huo ulitolewa na Meneja wa Kusimamia utaratibu wa Biashara Salum Mussa Haji alipokuwa katika mkutano na mawakala uliofanyika huko Kiembesamaki.

 

Alisema hatua hiyo itasaidia kufikia malengo ya kufanya biashara hizo kwa kuweza kuinua kipato chao na taifa kwa ujumla.

 

Meneja huyo alisemaa kampuni hiyo inawajibu mkubwa wa kuweka mazingira salama kwa wafanyabiashara hao ili kuona wanatekeleza majukumu yao kwa kufuata sheria za nchi.

 

Alisema lengo la mkutano huo ni kuwakumbusha mawakala hao kufahamu vitu vinavyohitajika katika uendeshaji wa biashara zao ikiwemo kukata leseni pamoja na kufuata taratibu nyengine za nchi.

 

Kwa upande wa Meneja wa Masoko na Mawasiliano wa Kampuni hiyo, Rukia Mtingwa, alisema mkutano huo wanafanya kila mwaka kwa mawakala wao ili kusaidia kutatua changamoto zinazowakabili pamoja na kuleta ufanisi katika utekelezaji wa wajukumu yao.

 

Alisema mawakala hukutana na changamoto kadhaa katika kazi zao ambazo husababisha kutofikia malengo yao hivyo kupitia kongamano hilo husaidia kutoa mchango mkubwa wa kutatua changamoto hizo.

 

Kwa upande wa afisa wa huduma ya Ezypesa Eunice Hubert, alisema kampuni hiyo imekuwa ikitoa huduma tofauti ili kuwarahisishia wananchi kuzitumia kwa urahisi pamoja na kuwaondoshea usumbufu.

 

Hivyo alitumia fursa hiyo kuitaka jamii kuzitumia huduma zinazotolewa na kampuni hiyo ili waweze kunufaika nazo na kuleta maendeleo pamoja na kukuza uchumi wan chi.

 

Kwa upande wa mawakala hao walitumia fursa hiyo kuiomba kampuni hiyo kutoa elimu ya kina kwa wananchi ili kufahamu huduma mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo.
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.