LIJUWE TATIZO LA KIZUNGUZUNGU (DIZZINESS)
LINAVYOISUMBUWA JAMII
Takribani kila mwaka watu milioni 8 huonana na
wahudumu wa afya kama madaktari na wanasaikolojia wao kutokana na kizunguzungu kisichoelezeka.
Tatizo la kizunguzuzungu
ni miongoni mwa matatizo sugu yanyowakumba watu wengi katika jamii, kimsingi tatizo hili
mara nyingi huwa ni ishara ya
tahadhari inayotolewa na mwili kuwa kuna kitu fulani hakiko katika hali ya usawa, hivyo uchunguzi wa chanzo cha tatizo
unapaswa kufanywa haraka. vile inavyowezekana.
NINI MAANA YA
KIZUNGUZUNGU?
Kizunguzungu ni tatizo ambalo linaweza kumpata mtu yeyote
na kuweza kupoteza utambuzi na uimara wa kiwiliwili chake. Kwa maana hiyo basi
kizungu ni tatizo la haraka/ghafla linalotokana
ukosefu wa kiasisi kidogo cha
oksijini kwenye ubongo/akili na kuweza kushindwa kuhimili mizigo wa mwili
husika na kuwa na udhaifu katika mwili,kichwa kuanza na stim za mihemko,koptea kwa usawa wa
mwili na moyo kupiga pole pole.
SABABU ZA
KIZUNGUZUNGU
Kizunguzungu si ugonjwa bali ni dalili ya ugonjwa .Ziko sababu nyingi sana
zinazompelekea mtu kupata/kusikia kizunguzungu katika maisha haya ya kila siku,
nazo ni:
Ukosefu wa damu mwilini,au kupunguwa kwa mwendo kasi wa
damu .Hali hii mara nyingi huwa wanapata
sana wanawake pale ambapo wapo kwenye
siku zao au wakati wa uja uzito hasa katika ile miezi mitatu ya mwanzo,kupungikiwa
kwa sukar mwilini,Ugonjwa wa presha,kukosekana kwa wa usingizi wa kawaida (insomnia),kuwa na
msongo wa mawazo,maumivu ya kichwa,kuwa mja mzito hasa katika miezi mitatu ya
mwazo,kwa baadhi ya wanawake kuwa kwenye mzunguko wao wa mwezi kwani wengi huwa wanapoteza damu nyingi ,kumwa
na unyusi baadhi ya magonjwa ya sikio kama vile uvimbe ndani ya sikio.ugonjwa
wa mishipa ya fahamu,kuwa kwenye hali ya mfadhaiko,kufa ganzi mwilini,kupata na
muangaza wa juwa kwa muda mrefu sana , kupungikiwa na maji mwilini.uvimbe
kwenye ubongo kunakosababishwa na maumivu makali ya kichwa,ugonjwa wa kifafa
ambao huambata na kupoteza ufahamu.ubigaji wa mastabesheni/ponyeto unaweza
kupelekea kupata kizunguzungu,kuna baadhi ya tafiti zimeonyesha watu wamelala
kwa muda mrefu kitandani kuna uwezekano mkubwa wa kupata kizunguzungu,na baadhi
ya matumizi ya dawa za kemikali au miti
shamba bila mpangilio maalumu.
DALILI NA ISHARA
ZA KIZUNGUZUNGU
Mtu mwenye
kizunguzungu hujisikia kama kichwa chake
kinazunguka zunguka,,kuyumba yumba, kujisikia mwepesi,kupunguwa nuru ya macho
kwa ghafla,maumivu mepesi ya kichwa kizima,kujisikia/kuhisi umepungikiwa na
pumzi mwilini,kuhisi marue rue,kuhisi kama unataka kuanguka,kupungukiwa kwa
nguvu za kuona,kujisikia mnyovu mnyovu,kusikia kichefu chefu ,kama
unatakutapika
MATIBABU YA KIZUNGUZUNGU
Tatizo la
kizunguzungu linaweza kudhibitiwa kutoka
na utambuzi wa kile kilichosababisha
kizunguzungu
Ø Hatua ya mwanzo unatakiwa
ukae kitako na kufumba macho ikibidi
hata kulala chini
Ø Kizunguzungu
kinachotokana na upungufu wa damu mwilini mara nyingi hali husababisha mwili kukosa hewa ya oksijeni ya kutosha. Kwa
maana hiyo mgonjwa anatakiwa atumie vidonge vyenye madini ya chuma na ulaji wa
mboga za kijani, maziwa, siagi na jibini husaidia kuondoa tatizo la
kizunguzungu
Ø kizunguzungu kinachotokana
kuwa na msongo wa mawazo dawa pekee ni kujipumzisha na kuacha kuwaza kwa
muda.ikiambatana na kufanya mazoezi mepesi mepesi ya kuvuta na kushusha pumzi
Ø Kunywa maji kwa
wingi hasa kwamba kizungunguzungu kimesababishwa na ukosefu wa maij mwilin alau lita moja na nusu ilikurejesha
virutubisho vilivyopotea kutokana na joto kali.
Ø Kizunguzungu
kilichosababishwa na ukosefu wa usinginzi, kinahitaji kushugulikiwa na mtaalamu
wa masuala ya usingizi au kutibiwa hospitali, ni vizuri kuwasiliana na daktari
mara moja kuhusu tatizo hilo.
Ø Upungufu wa damu mwilini (Anaemia), nao
husababisha kizunguzungu wakati mwingine, hali hii hutokana na mwili kukosa
hewa ya oksijeni ya kutosha. Kula vidonge vyenye madini ya chuma na ulaji wa
mboga za kijani, maziwa, siagi na jibini husaidia kuondoa tatizo la
kizunguzungu.
Ø Mwisho kabisa
kwa vyoyote ikiwa kizunguzungu kitazidi kuendellea kila uchao unatakiwa kuwaona timu ya madakitari kama vile,daktari wa kiwiwili,daktari wa
magonjwa ya akili, na mabingwa wa ushauri nasaha..
INDHARI
Itambulike kwamba sio kawaida kwa mtu
mwenye afya nzuri kuweza kusikia kizunguzungu kila mara, kwa
maana hiyo basi kama utajihisi unasumbuliwa na tatizo la
kizunguzungu kila wakati ujue una tatizo ambalo unashauriwa kulifikisha katika
hospital kwa uchunguzi zaidi.
USHAURI
Kwa kawaida,
tatizo la kizunguzungu unaweza kulidhibiti mwenyewe kwa kutumia tiba mbadala ya
kutengeneza mwenyewe nyumbani na kama tatizo litakuwa sugu, basi unashauriwa
kumuona daktari mapema zaidi kabla hali hajawa mbaya zaidi.Vile vile ni jambo zuri sana kwa kila mtu kujenga tabia
ya kupima afya yake kila inapobidi pamoja na kuchunguza mwenendo wa mwili na
kuchukua hatua za haraka za kudhibiti dalili zisizo za kawaida mwilini ili
kujiepusha na maradhi hatari yanayoweza kuhatarisha maisha ya binadamu..
Imetayarishwa
na:
Mohammed
Sharksy
Mkufunzi
Msaidizi,
Skuli
ya Afya Sayansi za Tiba,
Chuo
Kikuu cha Taifa cha Zanzibar, SUZA
0777432493
au email: mohammed.rashid96@yahoo.com,
ruruma96@gmail.com
No comments:
Post a Comment