Habari za Punde

Mbunge wa jimbo la Gando atoa msaada wa vigari vya walemavu - Wheelchairs kwa watu wenye ulemavu ndani ya jimbo lake

BAADHI ya watu wenye ulamavu kutoka Jimbo la Gando wakiwa na wazazi na ndugu zao, wakifuatilia kwa makini nasaha za Mbunge wa Jimbo la Gando Salimu Mussa Omar, kabla ya kukabidhi vigari vya magurudumu matatu kwa ajili ya walemavu.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

BAADHI ya vigari vya magurudumu matatu ambavyo vipo vinavyotumia umeme na visivyotumia umeme, vikikabidhiwa kwa watu wenye ulemavu ndani ya jimbo la gando Wilaya ya Wete.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MBUNGE wa Jimbo la Gando Kisiwani Pemba Salim Mussa Omar, akizungumza na wananchi, wazazi, walezi na watu wenye ulemavu kabla ya kukabidhi vigari vyenye magurudumu matatu hafla iliyofanyika hukpo Gando.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MBUNGE wa Jimbo la Gando Salim Mussa Omar, akimuweka sawa katika kigari cha magurudumu matatu kijana Khamis Ali Nuhu ambaye anaulemavu, baada ya kumkabidhi kigari hicho.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MBUNGE wa Jimbo la Gando Salim Mussa Omar, akimuendesha kijana Salim Abdalla (Injinia) mwenye ulemavu wa miguu katika kigari cha magurudumu matatu, baada ya kumkabidhi kigari hicho.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

MBUNGE wa Jimbo la Gando Salim Mussa Omar, akimuangalia kijana Salim Abdalla (Injinia) mwenye ulemavu wa miguu katika kigari cha magurudumu matatu, akikiendesha kigari hicho baada ya kumkabidhi kigari hicho.(PICHA NA ABDI SULEIMAN, PEMBA)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.