Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa akitoa maelekezo kwa COSOTA na BASATA
kuandaa mfumo wa kuuza kazi za Wachoraji na Wachongaji kwa njia ya mtandao
kufuatia ukuaji wa teknolojia na uwanda mpana wa masoko katika mfumo wa mtandao
au programu za simu ’Apps’ leo Machi 15,2021 Jijini
Dar es Salaam katika kikao wadau wa
Sanaa ya Uchoraji na Uchongaji kilicholenga kutatua changamoto zinazowakabili.
Katibu wa Tingatinga Arts Tanzania Bw. … akiwasilisha akimwomba Mheshimiwa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa kumsaidia kutatua changamoto ya mgogoro wa mipaka ya Kiwanja cha Ofisi yao Oysterbay leo Machi 15,2021 jijini Dar es Salaam katika kikao wadau wa Sanaa ya Uchoraji na Uchongaji kwa kilicholenga kutatua changamoto zinazowakabili.
Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe.Innocent Bashungwa ameagiza
COSOTA na BASATA
kuandaa mfumo wa kuuza kazi za Wachoraji na Wachongaji kwa njia ya
mtandao.
Mheshimiwa Bashungwa ametoa agizo hilo leo Jijini Dar es Salaam katika kikao chake na
Wasanii wa Sanaa ya
Uchoraji na uchongaji nchini kilicholenga kutatua changamoto
Zinazowakabili katika
uendeshaji wa kazi zao ikiwemo suala la masoko.
inatangaza biashara
kwa haraka zaidi na katika hili COSOTA mtatakiwa kuhakikisha mnalinda
Hakimiliki za kazi
hizo,"alisema Mhe.Bashungwa.
Akiendelea kuzungumza katika mkutano huo Waziri huyo aliwasihi Wachoraji na Wachongaji
kusajili kazi zao
COSOTA ili ziweze kulindwa, pia alitoa msisitizo kwa wadau hao kuhakikisha
wanawasiliana BASATA
pamoja na COSOTA pale wanapokuwa na mikataba yao kibiashara
kwa lengo la kupata ushauri wa kisheria ili kuweza kulinda kazi hiyo pamoja na maslahi yake.
Pamoja na hayo naye Afisa Mtendaji Mkuu na Msimamizi wa Hakimiliki Tanzania (COSOTA)
Bibi.Doreen Sinare alieleza
kuwa taasisi hiyo imetengeneza Kanuni mpya ambazo zitawasaidia
Wachoraji na
Wachongaji kunufaika na kazi zao baada ya kuuza kazi zao na kazi hizo kwenda
kuuzwa tena nje ya
nchi kupitia minada na njia nyingine kama hizo ambapo kazi huuzwa kwa
bei za juu ilihali
msanii kutokupata chochote kutokana na mauzo hayo zijulikanazo kama
‘resale royalties
rights’.
"Napenda kuwasisitiza kuhusu suala la kusajili kazi zenu kuna wakati nilitembelea ofisi za
Tingatinga na
nikawashauri kuhusu suala la kusajili kazi zenu COSOTA lakini baadhi yenu
walikuja
ila wengine hawakuja sasa naendelea
kuwasisitiza kusajili msisubiri mpaka mnapopata
changamoto ndiyo mnaanza
kuhangaika,"alisema Bibi.Doreen.
Pamoja na hayo Mtendaji huyo alieleza dhamira yake ya kutembelea eneo la biashara ya vinyago
Mwenge Machi 19, 2021 kwa lengo la kuwapa
elimu ya Hakimiliki na Hakishiriki ili kuwaongezea
uelewa wa masuala hayo
ikiwemo maboresho ya Kanuni mbalimbali zinazosimamia hakimiliki.
Pamoja na Kituo cha
Wachoraji wa Sanaa ya Tingatinga Oysterbay ambapo itakuwa ni mara
nyingine anawatembelea.
Mbali na hayo Bibi.Doreen alitangaza napenda kutoa ofa kwa wanawake wanaofanya kazi ya Sanaa ya
Ufundi kupamba Ofisi ya COSOTA kwa kazi zao ikiwemo
kwa Sanaa ya uchoraji au uchongaji
Kufuatia mgogoro wa Tingatinga Arts na Kampuni ya Kenya Mtendaji Mkuu wa
COSOTA aliwaelekeza
viongozi wa chama hicho kumpeleka mkataba wao katika Ofisi yake ili
aweze kutoa ushauri.
Pamoja na hayo Katika kikao Waziri Bahungwa alisisitiza mikataba huo
ufuatiliwe na COSOTA, na kama kuna haki za
Tingatinga basi haki hizo zifuafuatiliwe na
zipatikane hii ni kutokana na sintofahamu ya kusemekana kuwepo kwa baadhi ya wasanii ambao walisaini na kulipwa kwa kazi hiyo. Hivyo mkataba ndio utatoa picha kamili.
Kwa upande Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Bw.Andrian Nyangamale alitoa ombi kwa
Serikali kuwa anaomba
katika zawadi zile za vinyago au picha za kuchorwa zinazotolewa kwa
wageni Ikulu basi
Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ataje jina la aliyefanya
fanya kazi hiyo pale
anapokabishi. *Mh. Waziri alipokea na kuahidi kufanyia kazi jambo hilo.*
No comments:
Post a Comment