Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleiman Abdulla ameitembelea familia ya aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Marehemu Maalim Seif Sharif Hamad nyumbani kwao Mbweni Jijini Zanzibar kwa ajili ya kutowa pole na kuwafariji kufuatilia kwa msiba wa kuondokewa na mpendwa wao.
Makamu wa Pili wa Rais ameitaka familia hiyo kuwa na subra katika kipindi hiki pamoja nakuendeleza umoja na mshikamo aliouwacha marehemu Maalim Seif na serikali itaendelea kushirikiana na familia hiyo wakati wote.
Makamu wa Pili wa Rais alifutana na mkewe Mama Sharifa Omar Khalfan pamoja na viongozi wa wizara ya Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais sera, uratibu na baraza la wawkilishi.
No comments:
Post a Comment