Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi akutana na Uongozi wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithna Asheri Ikulu leo

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithna Asheri Bw. Aunali K.Khalfan akitowa maelezo ya Jumuiya hiyo wakati wa mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar na (kulia kwa Rais) Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo kutoka Uganda Kampala  Alhajj Shabir Najafi.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimsikiliza Bw. Munir Daya akitowa maelezo ya Kitabu cha Jumuiya hiyo kabla ya kumkabidhi, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.na (kulia kwake) Mwenyekiti wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithan Sheri Afrika kutoka Kampala Uganda Alhajj Shabir Najafi na Mamamu Mwenyekiti wa Bw. Aunali K.Khalfan a(Picha na Ikulu)

 RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithan Sheri walipofika Ikulu Jijini Zanzibar kwa mazungumzo yaliofanyika katika ukumbi wa Ikulu na (kulia kwa Rais ) Mwenyekiti wa Jumuiya ya Khoja Shia Ithna Sheri Afrika Alhaj Shabir Najafi kutoka Kampala Uganda akiongozana na Ujumbe huo.(Picha na Ikulu)

STATE HOUSE ZANZIBAR

OFFICE OF THE PRESS SECRETARY

PRESS RELEASE

  Zanzibar                                                               16.03.2021

---

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi ameikaribisha Jumuiya ya ‘Khoja Shia Ithna Ashir Jamaats of African’ na kuitaka kuzitumia vyema fursa za uwekezaji na biashara zilizopo Zanzibar.

 

Dk. Miwnyi alieleza hayo leo Ikulu Jijini Zanzibar wakati alipofanya mazungumzo na uongozi wa Jumuiya ya  ‘Khoja Shia Ithna Ashir Jamaats of African’ ukiongozwa na Mwenyekiti wake Alhaj Shabir Najafi kutoka Kampala Uganda.

 

Katika maelezo yake, Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imefungua milango yake katika sekta ya biashara na uwekezaji kwa ajili ya kukuza uchumi na kuimarisha maendeleo hapa nchini.

 

Hivyo, Serikali inawakabiribisha wawekezaji na wafanyabiashara wa Jumuiya hiyo kuzitumia fursa hizo kwa kuja Zanzibar na kufanya shughuli za uwekezaji na biashara ili kuiunga mkono Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika juhudi zake za kukuza uchumi na kuwaletea wananchi maendeleo.

 

Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa kwa vile uchumi wa Zanzibar hivi sasa umejikita zaidi katika uchumi wa buluu hivyo, ni vyema Jumuiya hiyo ikaangalia fursa zilizopo kupitia uchumi huo ili iweze kuja kuekeza na kufanyabiashara hapa Zanzibar.

 

Aidha, Rais Dk. Mwinyi aliueleza uongozi huo juhudi zinazochukuliwa na Serikali anayoiongoza katika kuimarisha na kukuza uchumi wa Zanzibar.

 

Sambamba na hayo, Rais Dk. Mwinyi aliipongeza Jumuiya hiyo kwa Juhudi zake za kuisaidia huduma za Kijamii zikiwemo huduma za afya, maji, elimu na nyenginezo.

 

Rais Dk. Mwinyi aliueleza uongozi huo kwamba bado wananchi wa Zanzibar wanahitaji huduma hizo za kijamii hivyo ni vyema wakaitumia fursa hiyo kuwasaidia ikiwa ni kwa lengo la kuiunga mkono Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwaletea maendeleo endelevu wananchi wake.

 

Nae Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Alhaj Shabir Najaf alimpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa hatua yake ya kuwakaribisha wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Jumuiya hiyo kuja kufanya shughuli zao hizo hapa Zanzibar.

 

Katika maelezo yake Mwenyekiti huyo wa Jumuiya ya ‘Khoja Shia Ithna Ashir Jamaats of African’ aliahidi kulifanyia kazi suala hilo kwa kupitia Jumuiya yao pamoja na kuzitangaza fursa zilizopo Zanzibar.

 

Mwenyekiti huyo pia, alieleza utayari walionao wa kusaidia huduma mbali mbali za kijamii zikiwemo huduma za maji, elimu, afya na nyenginezo.

 

Aidha, Alhaj Shabir Najaf alimueleza Rais Dk. Mwinyi mikakati iliyowekwa na Jumuiya yao katika kusaidia kutoa huduma za kijamii hapa Zanzibar.

 

Mapema Makamo Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Aunali Khalfan ambaye ni mzaliwa wa Zanzibar kwa niaba ya Jumuiya hiyo alimpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kishindo.

 

Hivyo, walimuombea kwa Mwenyezi Mungu kuendelea kumpa Rais Dk. Mwinyi afya njema pamoja na maisha marefu ili aendelee kuiongoza Zanzibar na wananchi wake.

 

Sambamba na hayo, Jumuiya hiyo ilitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kufanikiwa kisiasa kutokana na hatua yake ya kuwaunganisha Wazanzibari na kuwafanya kuwa kitu kimoja hali ambayo imepelekea kuwepo kwa amani, umoja na mshikamano hatua ambayo itaipaisha Zanzibar kiuchumi na kimaendeleo.

 

Katika maelezo yake Makamo Mwenyekiti huyo alieleza shughuli zinazofanywa na Jumuiya hiyo pamoja na azma waliyonayo katika kuiunga mkono Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwasogezea wananchi huduma za kijamii zikiwemo maji, elimu, afya na nyenginezo.

 

Jumuiya   hiyo iliyoanzishwa mwaka 1946 na kusajiliwa hapa Tanzania mnamo mwaka 1960 kwa kupitia  Jumuiya yake ndogo ya ‘Bilal Muslim Mission’ imeeleza azma yake ya kuisaidia Jamii kwa Unguja na Pemba katika kutoa huduma  zikiwemo za maji, afya, elimu pamoja na kuwawezesha wanawake wajasiriamali hasa wale wa vijijini.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 

 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.