Na. JaalaMakame Haji- ZEC
Zoezi la
Uchukuaji na urejeshaji wa fomu za uteuzi wa Wagombea wa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la
Pandani na Wadi ya Kinuni ambao utafanyika tarehe 28 Machi, 2021
limekamilika ambapo jumla ya Wagombea sita wamejitokeza kwa Uchaguzi wa Wadi ya Kinuni na Wagombea kumi Jimbo
la Pandani.
Akizungumza wakati wa urejeshaji wa fomu hizo msimamizi wa Uchaguzi Jimbo
la Pangawe Ndg.Suluhu Ali Rashid
alisema hatua inayofuata ni kufanya uteuzi wa Wagombea hao ili kufanya Kampeni katika Maeneo waliyoomba kuteuliwa mara baada ya kupewa uthibitisho wa uteuzi.
Bw.Suluhu aliwataja waliochukua na kurejesha fomu Wadi ya Kinuni kuwa ni Bi
Salama Rajab Masinga kupitia CCM, Ndugu.Kassim Ali Abdalla wa CUF, Ndugu. Hamad Hassan
Hamad ACT Wazalendo, Ndugu. Bakar Muhammed Abeid wa Chama cha Demokrasia, Ndugu.Maulid
Suleiman Fadhil wa Chama cha Demokrasia Makini na Ndugu. Zamir Ali
Mabrouk kutoka Chama cha UPDP.
Naye Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo
la Pandani Khamis Abdalla Hassan aliwataja waliochukua fomu na kurejesha kuwa ni Ndugu.Mohammed Juma
Ali wa CCM, Ndugu. Said Hamad Ali wa Demokrasia Makini, Prof. Omar Fakih Hamad
ACT Wazalendo, Ndugu.Massoud Ali Said Chama cha Wananchi CUF, na Ndugu. Ali
Jabir Khamis wa Chama cha ADC.
Wengine ni Ndugu.Khamis Faki Mgau Chama
cha NRA, Bi Asha Fumu Ali Cham cha UPDP, Ndugu. Ali Hamad Omar wa Chama cha ADA
TADEA na Ndugu. Mohammed Sharif Khamis kutoka Chama cha NLD.
Ndugu.Khamis Hassan
aliwataka wagombea watakaoteuliwa mara baada ya kuwekwa wazi kwa fomu za uteuzi kwa saa ishirini na nne kuendelea kudumisha
Amani ya nchi katika kampeni za uchaguzi hadi kumalizika kwa Uchaguzi huo.
Ndugu Khamis alieleza kuwa,
Kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Pandani na Wadi ya Kinuni zinatarajiwa kuanza tarehe
13 mpaka 26 Machi, 2021.
No comments:
Post a Comment