Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi amewaasa waandishi wa habari nchini kujadili juu ya hali uchumi ya wanahabari katika vyombo mbalimbali vya habari hapa nchini.
Akiongea katika kongamano la
majadiliano la Wadau wa Habari kwa Maendeleo ya Nchi kuelekea kilele cha Siku
Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani Mei 3, itakayofanyika Jijini Arusha Dkt.
Abbasi amesema wakati umefika kwa waandishi wa habari kutafakari na kujadili
uwezo wa kiuchumi kwa vyombo vya habari ambavyo vingi huanzishwa kwa malengo
binafsi.
"Uchumi wa wanahabari una hali
mbaya, mishahara midogo na mara nyingine hupokea mshahara huo baada ya miezi
sita, hawana bima wala pensheni; ni namna gani tutasaidia vyombo vya habari
kiuchumi"
Aidha amesema Serikali ipo tayari
kupokea mapendekezo na kuyafanyia kazi maoni, ushauri kutoka kwa wadau kwa
lengo la kutafuta ufumbuzi
Amewataka wanahabari kujadiliana
mfumo mzuri wa uendeshaji wa vyombo vya habari, na kwamba majadiliano hayo
yatoe mawazo au mapendekezo ili Serikali iweze kuyafanyia kazi.
Ameongeza kwamba Serikali ipo tayari
kupokea na kufanya mabadiliko ya kisera au kisheria iwapo patakuwa na hoja ya
msingi kwa manufaa ya Taifa.
Mmoja wa Waandishi wa Habari, ( jina
limehifadhiwa) amesema hali ya waandishi wa habari ni mbaya kiuchumi.
" Mimi nina miaka mitano (5)
sasa nahesabika kama correspondent na sio muajiriwa hivyo sina mkataba wala
mshahara, nalipwa kwa stories. Pia ninapotaka kwenda kutafuta stories, ofisi
inanituma lakini hakuna nauli, nategemea kupiga simu kwa mwenzangu aliyepo eneo
la tukio na matokeo waanahabari wanataka kwenda kwenye stori wanazotoa bahasha
ili kukidhi mahitaji yetu kiuchumi".
Akichangia hoja ya uchumi kwa vyombo
vya habari, Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF) Deogratius Balile
amesema vyombo vya habari vinaweza kuwa na uchumi endelevu iwapo
vitashirikishwa katika mipango ya maendeleo ya Taifa .
"Mathalan, kushiriki katika
kufahamisha umma malengo na mpango wa maendeleo wa taifa na pia nafasi yake
katika kutangaza mpango huo". Amesema Balile.
Dkt. Abbasi amewashukuru Shirika la
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali na
Wadau mbalimbali wa habari kwa kuandaa kongamano hilo na akashauri UNESCO
kuandaa makangomano mengine hata mata mbili au nne kwa mwaka kufanyika zaidi ya
mara mbili kwa mwaka ili kujenga uelewa katika tasnia ya habari.
No comments:
Post a Comment