Habari za Punde

Wizara wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto yapokea msaada wa chanjo kwa ajili ya Kipindupindu

Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Nassor Ahmed Mazrui (kulia) akipokea boksi la vifaa vya  usajili kwa ajili ya  chanjo ya kipindupindu inayotarajiwa kutolewa kuanzia Julai 3 hadi 7 katika shehia 56 ambazo huathirika na maradhi ya Kipindupindu mara kwa mara, huko Ofisini kwake Mnazimmoja .
Baadhi ya Vifaa walivyokabidhiwa Wizara ya Afya na Mwakilishi Mkaazi wa  Shirika la Afya Duniani (WHO) Andemichael Ghirmy kwa ajili ya kusaidia utoaji wa huduma ya  Chanjo ya Kipindupindu inayotarajiwa kutolewa kuanzia Julai 3 hadi Julai 7 katika shehia 56 ambazo huathirika  na maradhi ya Kipindupindu mara kwa mara Nchini
Mwakilishi Mkaazi wa  Shirika la Afya Duniani (WHO) Andemichael Ghirmy (katikati) akitoa ufafanuzi kuhusiana na vifaa mbalimbali alivyovikabidhi kwa Wizara ya Afya ikiwa ni msaada kwa ajili ya Chanjo ya kipindupindu, hafla iliyofanyika  Wizara ya Afya Mnazimmoja 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.