Habari za Punde

SHAKA: Hayupo wa Kuigombanisha Serikali ya CCM na Wananchi, Akemea Watendaji Kuvunja Sheria kwa Maslahi Yao, Atoa Maelekezo Mazito kwa DC Rungwe - CCM Blog

Rungwe, Mbeya

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesikitishwa na ongezeko la matatizo ya ujauzito na utoro yaliokithiri kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari katika Halmashauri ya Rungwe  kutokana kuchangiwa na vitendo vya rushwa na urasimu uliokithiri.


Kimesema ni ajabu katika Halmashauri hiyo kujiwekea utaratibu wa kuwapiga faini wazazi ambao watoto wao ni watoro au wamepata ujauzito ambapo wazazi ambao wanafunzi wao wamepeana ujauzito wanapigwa faini ya Sh. 245,000  kila mmoja.


Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa NEC ya CCM, Itikadi na Uenezi Shaka Hamdu Shaka ameo yeshwa kuchefushwa na vitendo hi yo wakati akiwa katika mkutano wa Shina namba 3 Kata ya Kandete, kijiji cha Mwela Busekelo mkoani hapa  na kumuagiza Mkuu wa wilaya ya Rungwe Dkt. Vincent Anney kusitisha utekelezaji wa uamuzi  wa Bodi za shule na  kurejeshwa kwa fedha zote  zilizokusanywa kama faini kwa waliowapa na waliopokea (wanafunzi) wa shule za sekondari na msingi.


"Hatuwezi kukomesha vitendo vya kuwapa mimba watoto wetu wa kike kwa kuendelea kutozana faini kwa wazazi wote, yaani mtu mwanaye anapewa mimba na pesa anatozwa (245,000) na mifuko 10 ya saruju pamoja na mtenda kosa hilo halafu wote wanarejea kwenye jamii" Alisema Shaka.


Amefahamisha kuwa jambo hilo  ni kinyume na sheria ya elimu na kwa namna yoyote haiwezekani kwa waliopewa dhamana ya kuisimamia na kutafsiri sheria kubadilisha maudhui na kutasiri wanavyotaka wenyewe.


"Maelekezo ya Chama, mkuu wa Wilaya sitisha utekelezaji wa uamuzi huu kwa shule zote, na fedha zote zilizokusanywa zirejeshwe kwa wahusika na hatua stahiki kwa mujibu wa sheria zichukuliwe kwa waliohusika na tupewe mrejesho ndani ya siku 7." Alisisitiza Shaka.


Shaka amefahamisha kuwa rushwa na urasimu ni vitendo na tabia ambazo hazitavumiliwa hata kidogo na CCM na serikali zake katika kuwaletea maendeleo endelevu wananchi  haitutakubali kuona baadhi ya watumishi, watendaji na viongozi waliokosa uadilifu wanawagombanisha na wananchi  watatendaji hao CCM itaielekeza serikali wapishe  mapema ili watanzania wengine wapewe dhamana hizo kuendeleza gurudumu la maendeleo.


"Niwaombe na nitoe raia kwa mawaziri, manaibu mawaziri na watendaji wote waliaminiwa na Rais Samia kumsaidia wanapokuja ziara mikoani washuke hadi vijijni kusikiliza wananchi kama anavyofanya Waziri Mkuu Majaliwa, huku kuna shida kubwa wasiridhike na ripoti za mapambio wanazopatiwa, washuke waje waone uhalisi itawasaidia sana kuwatathmini wasaidizi wao wa  ngazi za chini kama wanakidhi haja ya mbio za kuwaletea wananchi maendeleo" Amefahamisha Shaka.


Shaka amesema inasikitisha kuona mama mjane mwenye miaka 67 ambaye binti yake alipewa ujauzito na anapigwa faini 245,000 na mifuko 10 saruji, kinyume na sheria ya elimu huku mkurugenzi, Tarafa wapo lakini mtendaji wa kata anavunja sheria za nchi wanaeleana wakati  wananchi zaidi kuumia na  kuwarudisha nyuma kiuchumi.


"Waliopewa dhamana lazima mtafisiri kwa usahihi  sheria za nchi ili kutoibua kero zaidi kwa wananchi. Jamii iwalinde watoto ili wakue katika malezi mazuri na kupata elimu waje kutumikia nchi yao" alisema Shaka.


Hata hivyo katika katika kikao hicho wananchi walilalamikia utaratibu wa wao kutakiwa kununua mbolea toka kwenye maduka ya pembejeo ya maafisa ugani ndio wapewe mbolea iliyotokana na ruzuku ya serikali bila kufanya hivyo hawapati mbolea ya ruzuku jambo ambalo sio sawa.


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Daniel Chongolo na Sekretarieti yake ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anaendelea na ziara yake mkoani Mbeya.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.