Habari za Punde

Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza Wapata Mafunzo Kwa Vitendo Kuchangia ZSSF kwa Njia ya Kieletroniki.

Mkurugenzi  uendeshaji na Utumishi Ndg. Juma Ali Simai  akifungua Mafunzo ya uwasilishaji michango ya wanachama wa Mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF kwa njia ya kielektroniki kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.kuwa na mashirikiano ya pamoja kwa kuupokea na kuuzowea mfumo wa kielektroniki ili taarifa za waajiriwa wake ziendane na michango yao wanayoitoa.

Washiriki wa mafunzo wakiwa masomo kwa vitendo. 

Na RAYA HAMAD – OMKR.     

Washiriki wa mafunzo ya uwasilishaji michango ya wanachama wa Mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF kwa njia ya kielektroniki kutoka Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wametakiwa kuwa na mashirikiano ya pamoja kwa kuupokea na kuuzowea mfumo wa kielektroniki ili taarifa za waajiriwa wake ziendane na michango yao wanayoitoa

Mkurugenzi uendeshaji na utumishi ndugu Juma Ali Simai ameyasema hayo wakati akifungua mafunzo ya siku moja yaliyowashirikisha maafisa utumishi, wahasibu na maafisa tehama wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na taasisi zake kuhusiana na uwasilishaji michango ya wanachama wa ZSSF kwa njia ya kielektroniki kwenye ukumbi wa mkutano Migombani

Amewakumbusha washiriki hao kuwa kuwekwa kwao pamoja katika mafunzo hayo ni kujengwa uwelewa na kuzidisha uwezo katika majukumu yao kwa  kushirikiana pamoja  jambo ambalo litatoa fursa kwa watendaji hao kusaidiana pale ambapo kutatokea mabadiliko iwe ya kubadilishwa ofisi ama masuala ya kiutendaji

Aidha amwasisitiza washiriki hao kukaa na watumishi wote na kuwapa elimu juu ya kile walichojifunza “hakuna sababu ya mfanyakazi yoyote wa Ofisi hii kubaki nyuma ama kupitwa na mfumo huu kupitia simu za kiganjani ama komputa hapa ofisini ili kila mmoja wetu aweze kuona kama kuna mapungufu ama kukosekana taarifa sahihi za michango yake kupitia simu yake ataweza kufatilia kwa ukaribu na kuweka sawa taarifa zake “alisisitiza Mkurugenzi Juma

Mkurugenzi Juma amesema Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais itaendelea kutoa mafunzo kwa watendaji wake na taasisi zake kwa kila kada kila hali inaporuhusu na kwa mujibu wa mpango mkakati wa Ofisi hio

Nae meneja Tehama kutoka ZSSF Bw Ali Haji Ameir amesema mafunzo ya kujenga uelewa ni muhimu ukizingatia kuwa ZSSF imejipanga vyema na itakapofika mwezi wa Disemba 2021 itakuwa ndio mwisho  wa uwasilishaji michango kwa njia ya  kikawaida iliyozoweleka na badala yake taasisi za Serikali na mashirika binafsi  yatalazimika kuwasilisha michango ya wanachama kwa kufuata mfumo kwa  njia ya kielektroniki

Hivyo amesisitiza kuwa njia ya kisasa ya mfumo wa kielektroniki ya uwasilishaji michango ya wanachama wa ZSSF ni rahisi na salama zaidi  iwapo muwasilishaji atakamilisha taratibu za usajili kwa vile kwa kutumia njia ya mfumo wa kielektroniki  uwasilishaji michango unaweza ukafanyika muda wowote  

Washiriki wa mafunzo wamejifunza jinsi ya kuwasilisha michango ya wafanyakazi  kwa mfuko wa hifadhi ya jamii ZSSF, maslahi ya watendaji kuelea kustaafu, namna ya mwanachama mmoja mmoja wa mfuko kupata taarifa kwa kutumia simu ya kiganjani au komputa.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.