
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akipokea zawadi ya
ngao kutoka kwa mwenyekiti wa Shirikisho la Viwanda nchini (CTI) Paul Makanza
mara baada ya kumalizika hafla ya utoaji tuzo za Rais za wazalishaji bora wa
viwandani.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akiwa katika picha ya
pamoja na washindi watatu wa juu wa jumla wa tuzo za Rais za wazalishaji bora
wa viwandani wakati wa hafla ya utoaji tuzo hizo
uliofanyika Serena Jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akikabidhi tuzo kwa
mshindi wa kwanza wa jumla wa tuzo za Rais za wazalishaji bora wa viwandani
ambaye ni Tanga Cement wakati wa
hafla ya utoaji tuzo hizo uliofanyika Serena Jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza na
wazalishaji wa bidhaa za viwandani wakati wa hafla ya utoaji tuzo za Rais za
wazalishaji wa viwandani iliofanyika Serena Jijini Dar es salaam
Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akizungumza na
wazalishaji wa bidhaa za viwandani wakati wa hafla ya utoaji tuzo za Rais za
wazalishaji wa viwandani iliofanyika Serena Jijini Dar es salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. Philip Mpango amesema bado kasi ya ukuaji wa sekta ya viwanda
nchini ni mdogo na hivyo kuitaka Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana
na Shirikisho la Viwanda (CTI) kufanya tafakuri ya kina kupata suluhu ya
changamoto zinazokwamisha Sekta hiyo.
Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa hafla
ya utoaji wa Tuzo za Rais kwa wazalishaji bora wa viwandani nchini, hafla
iliofanyika katika hoteli ya Serena Jijini Dar es salaam.
Amesema bado bidhaa zinazozalishwa hapa
nchini hazijakidhi mahitaji ya wananchi na baadhi kutokidhi viwango vya soko
hivyo kuendelea kuagiza bidhaa za viwandani kutoka nje ya nchi. Makamu wa Rais
ametaja baadhi ya bidhaa zilizotumia gharama kubwa kwa kuagizwa kutoka nje ya
nchi mwaka 2020 kama vile shilingi bilioni 200 kutumika kuagiza bidhaa za
vitambaa ikiwa pamba inazalishwa hapa nchini.
No comments:
Post a Comment