STATE HOUSE
ZANZIBAR
OFFICE OF THE
PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Durban, Afrika Kusini 15.11.2021

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi
ametoa salamu za pole kwa Rais Mstaafu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Awamu ya Saba Mheshimiwa Dk. Ali Mohamed
Shein kufuatia kifo cha Kaka yake Mzee
Shein Mohamed Shein kilichotokea jana (Novemba 14,2021).
Katika salamu hizo za pole, Rais Dk. Mwinyi alieleza kusikitishwa kwake na
kifo hicho na kumtakia pole na ustahamilivu Rais Mstaafu Dk. Shein
yeye na familia yake katika kipindi hiki kigumu cha msiba.
Rais Dk. Mwinyi na familia yake wamemuomba
Mwenyezi Mungu amjaalie Marehemu Mzee Shein Mohamed Shein amlaze mahala
pema peponi, Amin.
Rais Dk. Mwinyi ametoa salamu hizo akiwa Jijini Durban,
nchini Afrika Kusini akisihiri ufunguzi
wa Mkutano wa Maonyesho ya Kukuza Biashara baina ya nchi za Afrika.
Imetayarishwa na Kitengo cha Habari,
Ikulu Zanzibar
No comments:
Post a Comment