Habari za Punde

Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan aelekea nchini Misri kwa Ziara ya siku 3


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango katika uwanja wa Ndege wa Dodoma kabla ya kuondoka nchini kuelekea Cairo, Misri kwa ajili ya Ziara ya Kiserikali ya siku tatu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango wakati akielekea kupanda Ndege kwenda Cairo, Misri kwa ajili ya Ziara ya Kiserikali ya siku tatu. PICHA NA IKULU
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono viongozi mbalimbali waliomsindikiza katika uwanja wa Ndege wa Dodoma wakati akielekea Cairo nchini Misri kwa ajili ya Ziara ya Kiserikali ya siku tatu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.