Habari za Punde

Kampuni ya Vinasaba kushirikiana na SMZ kwenye utafiti wa vinasaba

Waziri wa Afya , Ustawi wa Jamii , Wazee, Jinsia na Watoto Mhe, Nassor Ahmed Mazrui, akizungumza na Ugeni Uliyofika Wizarani kwake, kwa lengo la  kushirikiana kufanya Utafiti wa Vinasaba, mazungumzo hayo yamefanyika Ofisini kwake Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar.
Waziri wa Afya , Ustawi wa Jamii , Wazee, Jinsia na Watoto Mhe, Nassor Ahmed Mazrui, akimkabidhi zawadi ya Mlango Dr. Abasi Eneobong, aliyefika Wizarani hapo na Wageni wengine,kwa lengo la  kushirikiana na Wizara ya Afya , Ustawi wa Jamii , Wazee, Jinsia na Watoto kufanya Utafiti wa Vinasaba.
Waziri wa Afya , Ustawi wa Jamii , Wazee, Jinsia na Watoto Mhe, Nassor Ahmed Mazrui, akiwa na Mkoba wenye zawadi za Spaice ndani yake, ili kuwapatia wageni wake waliyofika Wizarani kwake Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar, kwa lengo la  kushirikiana na Wizara ya Afya , Ustawi wa Jamii , Wazee, Jinsia na Watoto kufanya Utafiti wa Vinasaba, (kulia) ni Dr. Abasi Eneobong akiwa na zawadi hiyo.
Baadhi ya Wageni waliyofika Wizara ya Afya , Ustawi wa Jamii , Wazee, Jinsia na Watoto, kwa lengo la kushirikiana na Wizara hiyo ili kufanya Utafiti wa Vinasaba, wakiagana na Waziri wa Wizara hiyo, Mhe, Nassor Ahmed Mazrui,

  Waziri wa Afya , Ustawi wa Jamii , Wazee, Jinsia na Watoto Mhe, Nassor Ahmed Mazrui,akizungumza na Waandishi wa habari (hawapo pichani ) baada ya kupokea Ugeni uliyofika Ofisini kwake wenye lengo la kushirikiana na Wizara ya Afya , Ustawi wa Jamii ,Wazee, Jinsia na Watoto kufanya Utafiti wa Vinasaba.

(PICHA NA MARYAM KIDIKO – MAELEZO .)

Na Khadija Khamis – Maelezo Zanzibar 14/01/2022.


Kampuni  inayochunguza vinasaba kutoka Marekani imesema ina azma ya kushirikiana na  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika masuala ya utafiti wa vinasaba 

.

Akiyasema hayo Mwenyekiti wa Kampuni ya kuchunguza vinasaba ( 54gene,Ine.) Dr Abasi Eneobong, alipofika na ujumbe wake, kuonana na Waziri wa Afya Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Mhe.Nassor Ahmed Mazrui, huko ofisini kwake, Mnazimmoja.


Alisema azma ya ujio huo ni kushirikiana na Wizara ya Afya katika masuala ya utafiti wa vinasaba  ili kufanyakazi kwa pamoja katika uchunguzi huo.


Aidha alisema  lengo la mazungumzo yao ni kufunga Mkataba wa mashirikiano ya pamoja katika utafiti wa vinasaba (Private,  Public, Partneship,PPP) ambao unatarajiwa kufanyika wiki mbili zijazo.


Nae Waziri wa Afya Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,Mhe.Nassor Ahmed Mazrui amesema uchunguzi wa vinasaba itasaidia kupata dawa sahihi za kutibu  maradhi mbali mbali katika jamii.


“Kwa  vile Zanzibar ni kisiwa,tumechanganya damu  za watu tofauti kutoka nchi mbali mbali za Arabuni, India, Uzunguni, China na  Afrika uchunguzi wa vinasaba utasaidia kutibu” alisema Waziri.

.

Alifahamisha kuwa hii ni fursa azimu ya  Wizara ya afya ambayo iliingojea kwa muda mrefu ya kuimarisha maabara kubwa ya utafiti iliopo Binguni .


Alieleza Zanzibar itakuwa Makao Makuu ya uchunguzi kutokana na ushirikiano wa kampuni hiyo na kuifanya iwe na hadhi ya kimataifa  jambo ambalo litasaidia Wazanzibar kupata  mafunzo ya utafiti pamoja na fursa za ajira ..

Kampuni ( 54gene,Ine.) ina matawi yake kutoka nchi mbali mbali ikiwemo Nigeria,Kenya, Marekeni Londan na nchi nyengine.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.