Habari za Punde

Mkoa wa Kusini Unguja Wakabidhi Cheti na Kombe.

WAZIRI wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Tabia Maulid Mwita ameupongeza Mkoa wa Kusini Unguja kwa jitihada na uzalendo wa kuratibu Mwenge wa uhuru na kuleta hamasa kubwa katika Mkoa huo.

Akizungumza na uongozi wa Mkoa huo  mara baada ya kukabidhi kombe na cheti ikiwa ni ishara ya  kuzindua mwenge  wa uhuru   katika uwanja wa Mwehe Makunduchi, hafla iliyofanyika huko ukumbi wa wizara ya habari migombani .

Alisema Mkoa huo umeleta hamasa kubwa kutokana na juhudi zilizofanywa kwa kushirikiana na Wizara ya Habari,Vijana Utamaduni na Michezo katika  kuimarisha shughuli za Kitaifa .

Aidha amemuomba Mkuu wa Mkoa kuendelea kushirikiana katika masuala mbali mbali hasa ya vijana katika kuwaletea maendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadid  Rashid amesema Mwenge wa Uhuru umewapa historia katika mkoa huo, sambamba na kuendelea kushirikiana katika shughuli za kitaifa ili kuona zinakwenda kwa ufanisi.

Katibu wa Mkoa wa Kusini Unguja Salum Kassim Ali amesema haikuwa rahisi lakini maandalizi mazuri,uweledi,ushirikiano na  waratibu kutoka tanzania bara  na wananachi   yameweza kufanikisha ipasavyo.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.