Na. Muandishi Wetu.
Bodi ya Mapato
Zanzibar (ZRB) imekichukulia hatua kituo cha kuuzia mafuta cha United Petroleum
(UP) kilichopo Fuoni kwa kukipa hati ya makosa iliyotokana na kushindwa kutumia
Mfumo wa kutolea Risiti za Kielektroniki (VFMS).
Hatua hiyo
imechukuliwa leo katika ukaguzi wa matumizi ya mfumo wa kutolea Risiti za
kielektroniki kwa kwa Vituo vinavyouza mafuta ya nishati na aina zote za
biashara Unguja na Pemba.
Afisa Uhusiano ZRB
Ndg. Badria Atai Masoud, amesema kuwa ZRB haitasita kuwachukulia hatua za
kisheria wafanyabiashara wote ambao wanakiuka agizo la Serikali, la kutumia
mashine za kutolea risiti za kielektroniki kwa lengo la kuweka kumbukumbu za
mauzo yao katika mfumo ambao unakubalika.
Bi. Badria
amesisitiza kuwa, ZRB itaendelea kusimamia sheria na kuwachukulia hatua wale
wote ambao hadi sasa hawatii agizo la Serikali pamoja na kuwasisitiza
wafanyabiashara wote kuendelea kutoa risiti kwa kila mauzo ya bidhaa au huduma
watakazokuwa wanauza katika biashara zao.
Kwa upande wake,
Meneja Uhakiki kwa walipakodi ZRB Ndg. Suwedi Mohamed Suwedi amesema kuwa kwa
mujibu wa kifungu cha 23 cha sheria za usimamizi wa kodi kinasema kuwa kila
mfanyabiashara anaeuza bidhaa au huduma ni wajibu wake kutoa risiti za
kielektroniki.
Hivyo kwa vile kituo
cha UP Fuoni Petrol Station kimeshindwa kutii agizo hili, ZRB imempatia hati ya
makosa ya shilingi milioni mbili (2,000,000/=) kama adhabu kwa kosa hilo.
Naye Meneja wa kituo hicho Ndg. Vuai Suleiman Vuai amekiri kuwa wamepokea barua kutoka ZRB inayowataka kununua mashine za VFD na kutoa risiti katika kila mauzo wanayoyafanya na kwamba mpaka sasa hawajanunua na kuanza kutumia mashi ne hizo.
No comments:
Post a Comment