Habari za Punde

Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Kujenga Mabwawa 14 na Hekta Elfu 10 za Umwagiliaji kwa Ajili ya Uzalishaji wa Mbegu Shilingi Bilioni 420 Kutumika.


Mheshimiwa Hussein Bashe Waziri waKilimo akizungumza wakati akifungua semina ya siku mbili iliyowahusisha wadau wa Sekta ya Umwagiliaji mjini Morogoro

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji,Bw, Raymond Mndolwa akizungumza wakati wa semina hiyo.
Picha ya Pamoja ya Wajumbe mbalimbali walioudhuria Semina hiyo Walioketi. Katikati ni Waziri waKilimo Mheshimiwa Hussein Bashe.

Na.Mwandishi Wetu - MOROGORO

Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe, amesema kwa Mwaka wafedha ujao Wizara yake itatumia Shilingi Bilioni 420 katika ujenzi wa Miundo mbinu ya Skimu za umwagiliaji ikiwemo Hekta elfu kumi kwa ajili ya uzalishaji wa Mbegu ambapo wadau wa sekta binafsi watapewa kipaumbele kwa ajili ya kuzalisha Mbegu, ujenzi wa mabwawa 14 yatakayokuwa na miundombinu ya umwagiliaji kwa matumizi ya kilimo na mifugo.

Aliyasema hayo leo Mjini Morogoro wakati akifungua semina ya siku mbili iliyowahusisha wadau wa Sekta ya Umwagiliaji mjini Morogoro, Waziri Bashe ameendelea kusema kuwa utekelezaji wa kazi hiyo utakwenda sambamba na kuanzishwa kwa Ofisi za Umwagiliaji za Wilaya nchi nzima pamoja nakuajiri wasimamizi wa Skimu za umwagiliaji watakaohusika kusimamia zoezi la ukusanyaji wa ada na tozo za umwagiliaji kwa uhakika.

Eneo lingine la kipaumbele kwa Waziri Bashe ni pamoja na kuwasaidia Wakulima Wadogowadogo kupataTeknolojia bora za kilimo cha umwagiliaji kwa bei nafuu ili waweze kupata tija na kuchangia ongezeko la mavuno katika sekta ya umwagiliaji, zoezi hilo litawahusu pia Vijana wanaojishughulisha na kilimo cha umwagiliaji.

Kwaupande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw,Raymond Mndolwa amewataka watumishi wote wa tume ya Taifa ya Umwagiliaji kufanya kazi kwa bidi na ubunifu ili kutimiza matarajio yaliyowekwa na serikali, akiamini taasisi yake inauwezo wakutekeleza majukumu yaliyopangwa na serikali kwa wakati, ufanisi na ubora unaotakiwa katika kuhudumia wananchi.

“ Nitamsapoti kila mtumishi aweze kutimi za wajibu wake, tumejipanga na lililopo mbele yetu tunaweza kulitekeleza”

Semina hiyo ya siku mbili imewashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo sekta binafsi, Wakulima wadogo, Wataalam waBenki, Vyama vya Ushirika, Wahandisi na Maafisa kilimo wa Wilaya ikiangazia namna ya kuboresha maeneo matatu muhimu katika kilimo cha umwagiliaji ,uzalishaji, huduma za u mwagiliaji na njia bora yakukusanya Ada naTozozaUmwagiliaji.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.