Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein
Ali Mwinyi ameipongeza Benki ya Dunia kwa kuendelea kuinga mkono Zanzibar
katika sekta mbali mbali za maendeleo.
Rais Dk.
Mwinyi ametoa pongezi hizo leo Ikulu Zanzibar, wakati alipofanya mazungumzo na
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Kusini mwa Afrika, Bi
Victoria Kwakwa aliyefika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha sambamba na kueleza
jinsi ya utekelezaji wa miradi iliyo chini ya Benki hiyo.
Katika pongezi
hizo, Rais Dk. Mwinyi alieleza kwamba Benki ya Dunia ina historia ya muda mrefu
katika kuiunga mkono Zanzibar kwenye sekta za maendeleo.
Rais Dk.
Mwinyi alisema kuwa Zanzibar ni miongoni mwa nchi zilizoathirika na Uviko-19
hasa kupitia sekta ya utalii ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika pato la
taifa.
Hata hivyo alisema
kwamba hivi sasa shughuli za utalii hapa nchini zimekuwa zikiimarika kila uchao
mara kutokana na kutokuwepo kwa janga la Uviko-19 hatua ambayo inapelekea
watalii kutoka nchi kadhaa duniani kuja kuitembea Zanzibar.
Aidha, Rais
Dk. Mwinyi alimueleza kiongozi huyo hatua zilizofikiwa na Serikali ya Mapinduzi
ya Zanzibar katika kuendeleza miradi ya elimu na afya inayotokana na fedha za Uviko-19
zilizotolewa na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), ili kushuhulikia huduma za
jamii.
Hivyo, Rais
Dk. Mwinyi alitumia fursa hiyo kuishukuru na kuipongeza Benki ya Dunia kwa
kuendelea kuisaidia Zanzibar katika miradi yake ya maendeleo huku akieleza
vipaumbele vilivyowekwa na Serikali yake hivi sasa katika kuimarisha
miundombinu ikiwemo barabara na bandari pamoja na kuimarisha sekta ya uchumi wa
buluu.
Alieleza jinsi
ya sekta ya Uchumi wa Buluu ilivyochukua nafasi kubwa katika sekta ya utalii, uvuvi,
kuwasaidia akina mama wanaojishughulisha na kilimo cha mwani, bandari pamoja na
sekta nyenginezo.
Rais Dk.
Mwinyi alieleza hatua zilinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
katika kuhakikisha zao la mwani linapata thamani na wakulima wake wanafaidika
na kilimo hicho ikiwa ni pamoja na kujenga kiwanda cha kusarifu mwani huko Chamanangwe,
kisiwani Pemba.
Alimueleza
Makamu huyo wa Rais jinsi Serikali anayoiongoza ilivyoweka kipaumbele na
kutilia mkazo uimarishaji wa sekta ya elimu, maji,miundombinu ya barabara
pamoja na huduma za kijamii huku akieleza juhudi zinazochukuliwa katika suala
zima la kuongeza nishati ya umeme hapa Zanzibar.
Sambamba na
hayo, Rais Dk. Mwinyi alimuhakikishia Makamu huyo wa Rais wa Benki ya Dunia
kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza uhusiano na ushirikiano
uliopo kati yake na Benki hiyo hasa kwa kutambua juhudi inazozichukua katika
kuiunga mkono Zanzibar kwenye sekta zake mbali mbali za maendeleo.
Nae Makamu wa
Rais wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Kusini mwa Afrika, Bi Victoria
Kwakwa alimueleza Rais Dk. Mwinyi jinsi Benki ya Dunia inavyofarajika na juhudi
za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuendeleza na kuimarisha miradi ya
maendeleo inayosimamiwa na benki hiyo.
Makamu huyo wa
Rais wa Benki ya Dunia alimueleza Rais Dk. Mwinyi hatua zinazochukuliwa na
benki hiyo katika kuhakaikisha Zanzibar inafaidia kwa mara nyengine tena na fedha
za utekelezaji miradi ya maendeleo kupitia dirisha jipya la Jumuiya ya
Kimataifa ya Maendeleo (IDA 20).
Katika
mazungumzo hayo, Bi Victoria Kwakwa alimuhakikishia Rais Dk. Mwinyi kwamba
Benki ya dunia itaendelea kuunga mkono miradi ya maendeleo iliyopewa kipaumbele
na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiwemo miundombinu ya barabara pamoja na
sekta nyenginezo.
Alieleza
kwamba Benki ya dunia imekuwa na ushirikiano mkubwa na Zanzibar katika Nyanja
mbali mbali za kijamaii na kiuchumi ikiwemo ujenzi wa miundombinu, elimu, afya,
mazingira na mengineyo mingi kupitia mpango wa mikopo nafuu.
Aidha, Bi
Kwakwa alimueleza Rais Dk. Mwinyi kwamba janga la Uviko-19 limeweza kuathiri
kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi kwa nchi kadhaa zinazotegemea sekta ya
utalii na kueleza matarajio yake kwamba Zanzibar itarudi katika hali yake ya
mwanzo.
Nae Waziri wa
Fedha na Mipango Saada Mkuya Salum ambaye alifuatana na kiongozi huyo pamoja na
ujumbe wake, alieleza jinsi mashirikiano mazuri yaliopo kati ya Benki ya Dunia
na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Makamu wa Rais
wa Benki ya Dunia anayesimamia Kanda ya Kusini mwa Afrika, Bi Victoria Kwakwa
yuko nchini kwa ziara ya siku mbili kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ambaye anachukua nafasi ya aliyekuwa
Makamu wa Rais wa Benki hiyo Dk. Hafez Ghanem ambaye amestaafu.
Imetayarishwa na Idara ya Mawasiliano,
Ikulu Zanzibar. OF
RESPONSIBILITY
No comments:
Post a Comment