RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amewaapisha viongozi
na watendaji mbali mbali wa Serikali kushika nyadhifa zao kufuatia uteuzi
aliofanya hivi karibuni.
Katika hafla hiyo iliofanyika ikulu Zanzibar, Rais Dk. Mwinyi amemuapisha Juma Makungu
Juma kuwa Naibu Waziri Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi pamoja na Masoud
Hussein Idd kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Ikulu.
Aidha, Dk. Mwinyi alimuapisha Dk.
Maua Abeid Daftari kuwa Kamishna wa Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Rashid
Ali Salim kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda
pamoja na Rajab Yussuf Mkasaba kuwa Mkuu wa Wilaya Kusini Unguja.
Hafla hiyo ya Kiapo ilihudhuriwa na
Viongozi mbali mbali wa Kitaifa na Chama cha Mapinduzi, akiwemo Jaji Mkuu wa
Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dk. Mwinyi Talib
Haji , Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena Ahmeid Said pamoja na Naibu Katibu
Mkuu CCM Zanzibar Abdalla Juma ‘Mabodi’.
Wengine ni Mufti Mkuu wa Zanzibar
Sheikh Saleh Omar Kaab, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid, Mawaziri,
Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Idrissa Kitwana Mustafa, Meya wa Jiji la Zanzibar
Mohamed Mahamoud Mussa, Wakuu wa Vyombo
vya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa Dini pamoja na Wanafamilia.
Imetayarishwa na Idaya ya Mawasiliano
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment