Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Nane ni
kuona kwamba kiwango cha ufaulu wa wanafunzi wa Skuli za Zanzibar unazidi
kuimarika kila mwaka katika mitihani yao ya Taifa.
Rais
Dk. Mwinyi aliyasema hayo leo katika hafla ya chakula alichowaandalia wanafunzi
waliofaulu vyema zaidi katika mitihani ya Taifa ya Kidato cha Nne mwaka 2021 na
Kidato cha Sita mwaka 2022, hafla iliyofanyika katika viwanja vya Ikulu ya
Zanzibar.
Kwa
mnasaba huo Rais Dk. Mwinyi alisema kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika
sekta ya elimu kwenye ujenzi wa miundombinu ya taasisi za elimu, kuzipatia
vitendea kazi vikiwemo vifaa vya kusomea na kusomeshea na utoa mafunzo kwa
walimu ili wapate mbinu bora za kufundishia.
Rais
Dk. Mwinyi aliwaahidi kuwapatia Kompyuta mpakato ‘laptop’ wanafunzi wote wa
Kitado cha Sita na Kidato cha Nne waliopata daraja la kwanza wa Unguja na Pemba.
Pia,
Rais Dk. Mwinyi aliwaeleza wanafunzi waliofaulu kidato cha Sita kwamba wote watapata
mikopo ya Elimu ya Juu na kusisitiza kwamba Serikali itahakikisha inaiwekea
mazingira mazuri bodi hiyo huku akiwaleza wkamba wana fursa ya kutumia bodi
zote mbili za mikopo ikiwemo ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais
Dk. Mwinyi alisisitiza haja kwa Wizara ya Elimu kufanya mashindano baina ya
Skuli na Skuli, Mikoa na Mikoa pamoja na Wilaya kwa Wilaya kwani ushindani
unaleta matokeo mazuri.
Katika kuzithamini juhudi za wanafunzi hao
Rais Dk. Mwinyi ametoa nafasi za udhamini wa masomo “Scholaship” kwa wanafunzi
30 waliofanya vizuri katika mitihani yao ili kuendelea na masomo katika vyuo
mbali mbali.
Alitoa pongezi kwa skuli binafsi ambazo nazo zimekwua zikifanya vizuri na
kuweza kuisaida Serikali katika kupunguza mzigo wa wanafunzi katika skuli
zilizopo za serikali.
Sambamba na hayo, aliahidi mafunzo na maslahi
kwa walimu na kuahidi kwamba Serikali anayoiongoza itahakikisha inayazingatia.
Nae Waziri wa Elimu Leila Mohamed Mussa
alieleza mikakati iliyowekwa na Wizara hiyo katika kuimarisha sekta ya elimu
huku akiwanasihi wanafunzi waliopata daraja la kwanza wa kidato cha Nne na Sita
kujitambua na kuthamini jambo hilo walilofanyiwa na Rais.
Nae Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Amali Ali Abdulgulam… alieleza kwamba mafanikio hayo yote yametokana
na mashirikiano ya pamoja kati ya uongozi wa Wizara hiyo, watendaji,walimu
pamoja na wazazi.
Nae Katibu mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Amali Zanzibar Ali Khamis Juma akitowa
Takwimu za uafaulu wa wanafunzi alisema Mtihani ya kidato cha nne ulifanyika
mwezi Novemba 2021 na matokeo yake yalitoka January 2022 ambao jumla ya
wanafunzi 15,569 walifanya mtihani
huo na wanafunzi 4,403 wamefanikiwa
kuendelea namasomo ya kidato cha tano Julai 2022.
Alifahamisha kuwa ufaulu wao ni kati ya daraja
la kwanza hadi la tatu na ni sawa na asilimia 28.3, kati ya wanafunzi hao ,wanafunzi 445 walipata daraja la kwanza
ambapo nisawa na asilimia 2.8 tu,
ambao 308 ni miongoni mwao ambao wamefika Ikulu ya Mnazimmoja hivi leo.
Alisema mtihani wa kidato cha sita ulifanyika
Mei 2022 na matokeo yake yalitokea mwezi Julai 2022 ambapo jumla ya wanafunzi
3,683 walifanya mitihani na wanafunzi 3,644 waliofaulu kuendelea na masomo kwa
ngazi ya elimu ya juu katika vyuo vya ndani na nje kwa fani zote ambazo
Serikali itawekea kipaumbele kulingana na mahitaji yake.
Alisema kuwa kati ya wanafunzi hao, wanafunzi
693 walipata daraja la kwanza, ambapo 542 ndio waliofika katika hafla hiyo ya
chakula na zawadi Ikulu Zanzibar.
Alisema takwimu za ufaulu kwa kidato cha nne
yamekuwa za kutia moyo mwaka hadi mwaka
kwa vile kuna ishara zilizowazi za kuimarika na hivyo kuifanya Zanzibar nayo
kuwa ni mshindani halisi kwenye matokeo ya mitihani katika mikoa ya hapa
nchini.
Katibu Mkuu huyo alisema kuwa Wizara inafanya
jitihada za makusudi kuona kuwa matokeo ya mitihani ya kidato cha 4 na 6 yanakuwa
mazuri na yenye kupendeza ambapo kuanzia mwaka huu, Wizara hiyo inakusudia
kuongeza ufaulu angalau kwa wastani wa asilimia 5 kwa kila mwaka.
“Matokeo yote haya ni mazuri sana na mara ya
kwanza kutokea tangu Mapinduzi matukufu ya Zanzibar ya mwaka 1964, matokeo haya
yamekuja chini ya uongozi wako mahiri wa Serikali ya Awamu ya Nane, nidhahiri
kuwa mafanikio yanakisi ile slogan yako ya uchaguzi kuwa ‘Yajayo yanafurahisha,
yajayo ni neema tupu’,alisema.
Rais Dk. Mwinyi pia alitoa zawadi kwa
wanafunzi waliofanya vizuri zaidi wakiwemo wanafunzi watatu waliopata kompyuta
mpakato ‘laptop’ akiwemo mwanafunzi
mwanafunzi bora katika Tahasusi ya ECA (Economic,Commerce na Account) Nasra Ali
Omar ambaye pia anaingia katika kundi la wanawake 10 bora Tanzania.
Imetayarishwa na Idara
ya Mawasiliano,
Ikulu Zanzibar.
No comments:
Post a Comment