Habari za Punde

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan Amekutana na Kuzungumza na Kiongozi wa Kitaifa wa Qatar.Sheikh.Tamim bin Hamad Al Thani

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na viongozi mbalimbali kabla ya kuanza mazungumzo na Kiongozi wa Taifa la Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, Doha nchini Qatar tarehe 04 Oktoba, 2022. Aidha, Mhe. Rais Samia pamoja na mwenyeji wake wamezungumzia masuala ya kuimarisha uhusiano na Biashara baina ya Tanzania na Qatar.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Kiongozi wa Taifa la Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi za Kiongozi huyo Doha nchini humo tarehe 04 Oktoba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Kiongozi wa Taifa la Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, Doha nchini humo tarehe 04 Oktoba, 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan  akiwa kwenye mazungumzo na Muanzilishi na Mwenyekiti wa Wakfu wa Qatar (Qatar Foundation ) Sheikha Moza binti Nasser, Doha nchini Qatar tarehe 04 Oktoba, 2022.
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.