JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI
Simuyamaandishi: “ZIMAMOTO KUU” SimuNambari: 255-26-23200243 Telefax: 255-26-23200243 BaruaPepe: fire.rescue@frf.go.tz Tovuti: www.frf.go.tz
DODOMA 07 Novemba, 2022
Ofisi ya Kamishna Jenerali Makao Makuu Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
1 Mtaa wa Zimamoto
S. L. P. 1509
41102 VIWANDANI, DODOMA
TAARIFA KWA UMMA
Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Kamishna Jenerali John Masunga, anaujulisha umma kuwa Majaliwa Jackson Samweli, ameshapokelewa na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Hivyo maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, tayari yameshatekelezwa.
Majaliwa anatarajiwa kuanza mafunzo ya Zimamoto na Uokoaji pamoja na ya Uaskari katika Chuo cha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kilichopo Chogo Wilaya ya Handeni Mkoa wa Tanga.
Ikumbukwe kuwa tarehe 06 Novemba, 2022 ilitokea ajali ya kuanguka kwa Ndege ya Precision Air katika Ziwa Victoria, ajali hii ilisababisha majeruhi na vifo. Majaliwa alionesha ujasiri wa hali ya juu, kwa kuokoa wahanga 24 wa tukio hilo.
Kamishna Jenerali anatoa shukrani za dhati kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Taasisi za Umma na Binafsi, pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Kagera kwa ushirikiano mkubwa waliotoa katika zoezi la uokoaji katika ajali hiyo.
Kamishna Jenerali anatoa pole kwa Wafiwa wote na kuwaombea faraja katika kipindi hiki kigumu wanachopitia, anawatakia majeruhi wote afya njema.
Anawasihi Wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika kuokoa Maisha ya watu na mali dhidi ya majanga mbalimbali,
Imetolewa na;
SACF - Puyo Nzalayaimisi
Msemaji wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji
Makao Makuu Dodoma
07 Novemba, 2022
No comments:
Post a Comment