Habari za Punde

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Azindua Huduma za Afya katika Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kuzindua Huduma za Afya baada ya maboresho yaliyofanywa katika hospitali ya wilaya ya Kisarawe akiwa katika siku ya tatu ya ziara ya Mkoa wa Pwani, Novemba 29, 2022.  Wengine pichani kutoka kushoto ni Mganga Mkuu wa wilaya ya Kisarawe, Dkt.  Zaituni Hamza, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Dkt. Selemani Jafo,  Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge na kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI, Dkt. Festo Dugange.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akizungumza na wanawake waliokuwa wakisubiri kupata huduma katika hospitali ya wilaya ya Kisarawe wakati alipozindua Huduma za Afya hospitalini  hapo na kuwasalimia wananchi akiwa katika siku ya tatu ya ziara ya Mkoa wa Pwani.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.