Habari za Punde

Mhe.Gekul aiagiza Bodi ya Filamu kupitia Upya Katiba ya Shirikisho la Filamu

 

Na Shamimu Nyaki

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul Januari 23, 2023  Ofisini kwake Mtumba Dodoma  amekutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya viongozi wa Shirikisho la Filamu Nchini.

Katika kikao hicho Naibu Waziri Gekul, amepokea changamoto na mapendekezo kuhusu namna bora ya kuboresha uendeshaji na utendaji wa Shirikisho na Vyama vinavyounda Shirikisho hilo.

Mhe. Gekul, ameelekeza Bodi ya Filamu na Baraza la Sanaa la Taifa kupitia upya Katiba ya Shirikisho hilo pamoja na Vyama vyote ili kuangalia mapungufu na kuyafanyia kazi.

Aidha ameagiza Bodi ya Filamu pamoja na BASATA kukutana na viongozi wa Shirikisho na Vyama hivyo  kwa lengo la kuimarisha utendaji na ufanisi wa Shirikisho na Vyama vyake.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.