SERIKALI
ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema imekusudia kuifanyia mageuzi makubwa sekta ya
michezo visiwani kwa kujenga viwanja vya kisasa vinavyoendena na hadhi ya miaka
59 ya Mapinduzi.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,
Dk. Hussein Ali Mwinyi ameyasema hayo alipoweka jiwe la msingi la viwanja vya
michezo, Matumbaku, wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja
unaosimamiwa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, (ZSSF).
Dk. Mwinyi aliiagiza bodi ya Mfuko wa ZSSF kuharakisha
ujenzi ili ukamilike kwa wakati na wananchi wapate huduma wanazostahiki
Aidha, aliiamuru bodi hiyo kuikopesha fedha serikali ili
wakamilishe kwa wakati maeneo yote ya ujenzi wa viwanja hivyo vikiwemo viwanja
vya mpira wa mikono, (basketball netball, handball na volball) ambavyo vilikua nje
ya bajeti na kuahidi fedha zote watakazotumia serikali itawarejeshea.
Akizungumzia fedha za serikali za ahuweni ya uviko 19,
Dk. Mwinyi alieleza, fedha zote serikali imezielekeza kwenye miradi mikubwa ya
jamii ikiwemo Elimu, Afya, Maji safi na salama, umeme na kuwawezesha wananchi
kiuchumi, hivyo mradi wa viwanja vya michezo Matumbaku unatekelezwa kwa pesa za
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na sio fedha za uviko 19.
Alisema Serikali imelitumia eneo la
Matumbaku kuweka ujenzi huo baada ya eneo la zamani la Malindi kupisha ujenzi
wa maegesho ya magari na kutuo cha kisasa na mabasi, Aidha Dk. Mwinyi alieleza,
kuna mradi mwngine unaojenga barabara za lami na kazi zake zimeanza rasmi
kwenye maeneo mbalimbali ya mji.
Makamo wa Pili wa Rais, Hemed Suleiman Abdulla wakati akizungumza kwenye hafla hiyo, aliwataka viongozi na wananchi wa Zanziabr kwa pamoja kuzungumza lugha moja ya maendeleo, hivyo aliwaomba watendaji na wasimamizi wa mitadi yote ya maendeleo waikamilishe kwa wakati ili wananchi waendeelee kufurahia matunda ya Mapinduzi.
Aidha, alieleza miradi yote iliyozinduliwa na kuwekewa mawe ya msingi ni ya
mda mfupi pia ni jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya nane ya Dk.
Hussein Mwinyi na kuongeza kuwa mafanikio ya miradi hiyo ni utekelezaji wa
ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi 2020 /2025.
Naye, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Dk.
Saada Salum Mkuya, alisema ujenzi wa viwanja hivyo umegharimu shilingi bilioni
1.1 nakuongeza kuwa serikali imefanikiwa kuokoa shilingi bilioni 1.4 kwa
kutumia wakandarasi wa ndani ambao ni Jeshi la Kujenga Uchini nchini, JKU kwa
kuhakikisha ujenzi wa kiwango cha juu kabisa.
Katika hatua nyengine, Waziri wa Habari Utalii Vijana na
Michezo, Tabia Maulid Mwita alieleza ujenzi wa viwanja hivyo ni hatua ya kupigiwa
mfano kwani fedha zake hazikutokana na ufadhili wowote bali ni fedha za
Serikali kutoka ZSSF.
Akizungumza kwenye sherehe hizo, Katibu Mkuu wa Wizara ya
Fedha na Mipango, Dk.Juma Malik Akili alisema ujenzi wa viwanja hivyo ni upishwaji wa miradi mitatu mikubwa ya
maendeleo kwenye viwanja vya zamani vya michezo, Malindi ukiwemo ujenzi wa kituo
cha mabasi cha kisasa, ujenzi wa maegesho ya magari na ujenzi kituo cha mabasi
Kijangwani, hivyo alieleza ujenzi wa kisasa wa viwanja vya michezo, Matumbaku ni
uimarishwaji wa sekta ya michezo nchini na kuwaondoshea wananchi usumbufu kutokana na
kuhamishiwa viwanja vyao vya awali.
Alisema tayari Serikali imewapatia ZSSF eneo la Malindi
kwajili ya uwekezaji huo pamoja nakusubiri taratibu za mwongozo wa michoro kutoka
Mamlaka ya mji Mkongwe ili wakamilishe mradi huo.
Mradi
mpya wa viwanja vya kisasa, Matumbaku ulianza
Julai mwaka jana baada ya kuingia makubaliano na ZSSF na ulitarajiwa
kukamilika Oktoba mwaka jana lakini ulichelewa baada ya baadhi ya vifaa
vilivyoagiziwa kutoka nje ya nchi kutofika kwa wakati.
KITENGO
CHA MAWASILIANO,
IKULU
No comments:
Post a Comment