Dar es Salaam, 10 Februari 2023
Waziri
wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax
(Mb.) amepokea nakala za Hati za Utambulisho za mabalozi wateule wa nchi za
Misri na Marekani.
Mhe.
Waziri Tax amepokea nakala za hati za utambulisho za Balozi wa Misri nchini,
Mhe. Sherif Abdelhamid Ismail na Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Michael Battle
jana jioni katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza
na mabalozi hao kwa nyakati tofauti mara baada ya kupokea nakala zao za hati za
utambulisho, Dkt. Tax amewahakikishia ushirikiano kutoka Serikalini wakati wote
wa utekelezaji wa majukumu yao hapa nchini na kuwasihi kuendeleza ushirikiano
mzuri uliopo baina ya Tanzania na nchi zao.
Balozi mteule wa Misri nchini, Mhe. Sherif Abdelhamid Ismail ameahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya Misri na Tanzania katika sekta za nishati hususani mradi wa bwawa la mwalimu Nyerere, kilimo, biashara na uwekezaji.
“Misri
na Tanzania tunayo mengi ya kushirikiana, tunaahidi kuendeleza ushirikiano wetu
kwa maslahi mapana ya pande zote mbili, wakati wa utumishi wangu hapa Tanzania
nitaendeleza kwa maslahi mapana ya wananchi wetu wote,” alisema Balozi
Ismail
Kwa
upande wake Balozi Mteule wa Marekani, Mhe. Michael Battle amesema Marekani na
Tanzania zimekuwa marafiki wa muda mrefu, na itaendelea kushirikiana na
Tanzania katika sekta za Utalii, Kilimo, afya, biashara na uwekezaji pamoja na sekta
nyingine za kimkakati.
“Ni
furaha kwangu kuwepo hapa leo na kukabidhi nakala ya hati ya utambulisho wangu
hapa nchini Tanzania, napenda kuahidi kwa kipindi nitakachokuwa hapa
nitahakikisha kuwa uhusiano wetu wa kidiplomasia unakuwa na kuimarika kwa
maslahi ya mataifa yetu,” alisema Balozi Battle.
Imetolewa
na:
Kitengo
cha Mawasiliano ya Serikalini
No comments:
Post a Comment