Habari za Punde

HUduma za Afya Zafika Vijijini

Na Fauzia Mussa    Maelezo Zanzibar

Wizara ya Afya Zanzibar kwa kushirikiiana na Pharm Access international imeanzisha mpango maalum wa kuwafikia wagonjwa wa maradhi yasioambukiza katika ngazi ya jamii na kuwapatia elimu pamoja na huduma za Afya.

Hayo yamesemwa na  Afisa wa mradi wa wagonjwa wa maradhi yasioambukiza Queen-Ruth Msina wakati alipokua akifanya  mahojiano katika zoezi la utoaji wa huduma za  Afya kwa ngazi ya jamii lililofanyikaa  Koani Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.

Amesema  mradi huo ulianzishwa kufuatia  uwepo wa  changamoto za wagonjwa na madaktari wakati wa utoaji wa huduma za Afya ambao umelenga kutatua changamoto hizo  .

Aidha alifahamisha kuwa madaktari wamekua wakielemewa na wingi wa wagonjwa Vituoni jambo linalorejesha nyuma  jitihada za kuwahudumia wagonjwa wa maradhi hayo   kwa ufanisi kwani   muda wa kuwasikiliza huwa hautoshelezi.

Amefafanua kuwa wagonjwa wamekuwa wakitoka masafa marefu  na kukaa muda mrefu vituoni kusubiri huduma  jambo  linawapa ugumu  kufuatilia huduma  za Afya kwani wengi wao huwa ni wazee wasiojiweza.

Amesema mradi huo  unawakutanisha Madaktari na Vikundi vya Wagonjwa wenye maradhi yasioambukiza kwa mwezi mara moja katika Vijiji vyao ambapo wagonjwa hupatiwa elimu  na kubadlishana mawazo juu ya maradhi hayo.

"Tumeona wagonjwa wanapata shida kukaa foleni, na wanatoka Masafa marefu jambo linalwarejesha nyuma kurudia tena  Kliniki kupatiwa huduma ,mrad huu utawakutanisha wagonjwa na madaktari katika ngazi ya jamii na kuwaweka huru katika kuzungumza changamoto zinazowakabili. " alisema

Mapema Afisa huyo aliishauri jamiii kutokupuza  kuhudhuria  katika vikao ndani ya  shehia zao mara tu wanapotakiwa kufika ili kupata fursa kama  hizo    kwani zina tija na faida kwao.

Nao wanakikundi cha maradhi yasioambukiza cha Koani wameishukuru Wizara ya Afya kw kushirikiana na  Pharm Access kwa kuwasogezea huduma  za Afya  karibu na kuahidi kuzifatilia huduma hizo mara tu zinapofika katika jamii.

Jumla ya vikundi 25 vya wagonjwa wenye maradhi yasioambukiza vinatarajiwa kunufaika na  Mradi huo Unguja na pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.