Habari za Punde

Mkutano wa Hadhara wa Chama cha ACT-Wazalendo Viwanja vya Alabama

 

Makamu Mwenyekiti wa  Chama cha ACT -Wazalendo Zanzibar ambae pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungunza na kufurahia jambo na Mwenyekiti wa Chama Cha ACT-Wazalendo Mhe. Juma Duni Haji, wakati wa mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika katika viwanja vya Alabama Wilaya ya Mjini Unguja.Jimbo la Kikwajuni Zanzibar. 
Makamu Mwenyekiti wa ACT Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman akizungunza katika mkutano wa hadhara wa chama hicho kabla ya kumkaribisha mwenyekiti kuhutubia katika viwanja vya alkama Kikwajuni mjini Unguja.
Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Mhe.Juma Duni haji akizungunza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya alabama katika jimbo la kikwajuni Wilaya ya Mjini Unguja

Wanachama  wa Chamna cha ACT-Wazalendo wakifuatilia hutuba ya Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo Taifa Mhe.Juma Duni haji huko katika viwanja vya alabama jimbo lakikwajuni mjini Unguja

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha ACT –Wazalendo Zanzibar ambae ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amewataka Wazanzibari wote kuendelea kuungana na kuwa wamoja katika kutetea  haki sawa na kuendeleza  kuijenga Zanzibar yenye umoja na maridhiano jambo litakaloleta  Zanzibar mpya yenye neema na maendeleo kwa wote.

Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ameyasema hayo Viwanja vya Alabama  Jimbo la Kikwajuni wilaya ya mjini Unguja katika mkutano wa tatu wa hadhara wa chama hicho Kwa upande  wa Zanzibar.

Mkutano huo ni muendelezo wa mikutano ya hadhara ya chama hicho tokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kuruhusu kuendelea kwa mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa  nchini ambayo ilipigwa marufuku kwa takribani kipindi cha miaka saba iliyopita.

Mhe. Othman amesema kwamba Maono ya ACT ni kutetea na kujenga Zanzibar mpya yenye  neema   na kujenga  umoja bila kubaguana kwa kuzingatia kwamba Zanzibar inaasili ya watu mchanganyiko  kutoka makabila na nchi tofauti  tokea kipindi cha kabla ya uhuru wa mwaka 1964.

Mhe, Makamu amefahamisha kwamba katika kuthibitisha kuwepo  hali hiyo ya mchanganyiko mkubwa wa watu wa aina na makabila tofauti  tokea asili, kesi ya mwanzo iliyofunguliwa mahakamani katika kipindi cha kabla ya mwaka 1964 ni mama mmoja wa Zanzibar kudai mahakamani haki za watoto wake aliozaa na mwanaume mwenye asili ya kihidi.

Aidha amesema kwamba katika kipindi cha kabla ya mwaka 1964  Zanzibar ilikuwa na askari wapatao 707 ambao zaidi ya nusu walitoka katika makabila na nchi  tofauti  ambao miongoni mwa hao ndio walioendelea kuishi Zanzibar hadi sasa na kwamba hakuna sababu ya kubaguana.

Kwa upande mwengine Mhe. Othman amesema kwamba chama hicho kitatimiza wajibu wake wa kuwasemea wananchi  katika masuala mbali mbali yanayowahusu kupitia mikutano ya hadhara bila kumuonea haya ama aibu mtu yoyote samabamba na kuwepo na kutetea umoja na maridhiano ya kweli.

Kwa upande mwake Mwenyekiti wa Chama hicho taifa Mhe. Juma Duni Haji (babu Juma), amewataka wazanzibar kuitumia fursa ya kuundwa Kikosi kazi cha  Kukusanya maoni ya Katiba mpya kwenda  kutoa maoni ya katiba inayohitajika itakayosaidia kuwepo pia muungano wenye haki  na maslahi sawa kwa pande zote mbili.

Aidha Mwenyekiti huyo pia alisisitiza haja ya wanzanibari kuitumia fursa hiyo katika kudai haki za Zanzibar kwenye muungano kupitia katiba mpya ikatakayopendekezwa ili kusaidia  kufikia malengo ya chama hicho kuleta umoja na maridhiano ya kweli miongoni mwa wazanzibari.

Amewakumbusha wazanzibari kukiunga mkono chama hicho kwa  vile  chama chake kunaamini maridhiano ya kweli  na  kutetea umoja miongoni mwa wazanzibari jambo litakaloleta maslahi ya kiuchumi na kuimarisha huduma biora za kijamii na kimaendeleo yakiwa ndio malengo halisi ya Mapinduzi ya mwaka 1964.

Mapema Naibu Mkurugenzi wa Chama hichi wa Haki za Binadamu na Makundi Maalum Pavu Abdalla Juma, amesema kwamba Zanzibar imekabiliwa na changamoto kubwa ya kuwepo vitendo vya udhalilishaji kwa wanawake na watoto jambo ambalo linaendelea kuleta athari kubwa kwa jamii ya wazanzibar na kwamba kunahaja kubwa ya kuungana katika kupambania tatizo hilo.

Mwisho

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Zanzibar kupitia Kitendo chake cha Habari leo tarehe 21.05.2023.

Kwa mawasiliano ya Haraka tafadhali

Piga simu.+255777424877  or  0774419740

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.