Habari za Punde

Rais Dk Hussein Mwinyi ahutubia Maadhimisho ya siku ya mwani Zanzibar leo 23/07/2023

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi wakimsikiliza Mkulima wa Mwani wa Kijiji cha Dimani Bi.Mwatima Abdalla Ali akionesha jinsi ya upandaji wa mwani katika maji, wakati akitembelea maonesho ya bidhaa za Mwani wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-7-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakipata maelezo ya bidhaa za mwani kutoka kwa Bi. Stella Kileo,akitembelea maonesho ya bidhaa mbalimbali zinazotokana na Mwani, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-7-2023 na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Mhe.Suleiman Masoud Makame .(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakipata maelezo kutoka kwa Mwanafunzi wa Taasisi ya Sazani Associates. Shayman Salum, jinsi ya kutengeneza juisi ya mwani na uji, wakati akitembelea maonesho ya bidhaa mbalimbali zinazotokana na Mwani, katika Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-7-2023 na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Mhe.Suleiman Masoud Makame .(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakipata maelezo ya bidhaa za mwani kutoka kwa Bi. Renae  Bruce Miller wa Mwani Mama East Africa Seaweed , wakati akitembelea maonesho ya bidhaa mbalimbali zinazotokana na Mwani, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-7-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa na Mkewe Mama Mariam Mwinyi, wakipata maelezo ya bidhaa za mwani kutoka kwa. Pili Mkemi wa Kikundi cha Wanawake Wanaojishughulisha na Uvuvi na Mwani  ( COWOFO ) wakati wakitembelea maonesho ya bidhaa mbalimbali zinazotokana na Mwani, katika Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyofanyika katika viwanja vya hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-7-2023 na (kushoto kwa Rais) Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Mhe.Suleiman Masoud Makame .(Picha na Ikulu)
BAADHI ya Wageni Waalikwa na Wakulima wa Mwani Zanzibar wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza katika ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-7-2023, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyoadhimishwa katika ukumbi huo leo.(Picha na Ikulu)
BAADHI ya Viongozi wa Idara mbalimbali za Serikali na Taasisi za Umma wakifuatilia hutuba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi (hayupo pichani) akizungumza katika ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-7-2023, wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyoadhimishwa katika ukumbi huo leo.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhi TUZO Maalum Mlezi wa Wakulima wa Mwani Kitaifa, Mwenyekiti wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mama Mariam Mwinyi, wakati wa hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar, iliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 23-7-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa TUZO Maalumu ya Mchango wake katika Kilimo cha Mwani Zanzibar, akikabidhiwa na Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar Mhe. Suleiman Masoud Makame na (kulia kwa Rais) Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mariam Mwinyi, wakati wa hafla ya Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyofanyika katika ukumbi wa  hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 23-7-2023.(Picha na Ikulu)
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Mwani Zanzibar yaliyofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Golden Tulip Uwanja wa Ndege Kiembesamaki Wilaya ya Magharibi “B” Unguja Jijini Zanzibar leo 23-7-2023.(Picha na Ikulu)
 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.