Habari za Punde

Zoezi la mavuno ya pweza Pongwe



Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi tarehe 14/10/2023 ilijumuika na wananchi wanaoishi pembeni ya eneo tengefu la ufugaji wa pweza, Pongwe, kwa mavuno ya msimu wa Julai-Septemba, 2023.

Ufunguaji wa mavuno hayo ulishuhudiwa na Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Kati, Bi Marina Joel Thomas, Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Dr Aboud Suleiman Jumbe na Mkurugenzi wa Idara ya Uhifadhi wa Maeneo ya Bahari, Dr Makame O Makame.
Zoezi la uvunaji linaendelea kwa siku tatu hadi Jumatatu tarehe 16 Oktoba 2023, na kuwa mpaka mwisho wa siku ya kwanza, tayari tani 3 za pweza zilikuwa zishavunwa na kufikia thamani ya soko ya zaidi ya Shilingi Milioni 30
Tanzania ni nchi ya kwanza inayozalisha pweza katika ukingo wa magharibi wa bahari ya hindi na kuwa kwa wastani nusu ya mavuno hayo yanatoka Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.