Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Mwinyi Azungumza na Uongozi wa Jumuiya ya Shia Tanzania Ikulu Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Uongozi wa Jumuiya ya Shia Ithnaasheri Tanzania ukiongozwa na Sheikh.Mkuu wa Jumuiya hiyo Maulana Sheikh.Hemed Jalala (kulia kwa Rais) walipofika Ikulu Jijini Zanzibar  kwa mazungumzo na kumpongeza, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 30-5-2024
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na Ujumbe wa Uongozi wa Jumuiya ya Shia Ithnaasheri Tanzania ukiongozwa na Sheikh.Mkuu wa Jumuiya hiyo Maulana Sheikh.Hemed Jalala (kulia kwa Rais) walipofika Ikulu Jijini Zanzibar  kwa mazungumzo na kumpongeza, mazungumzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Zanzibar leo 30-5-2024
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikabidhiwa zawadi maalum ya Kitabu na Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Shia Ithnaasheri Tanzania Maulana Sheikh Hemed Jalala , baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 30-5-2024
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiangana na Ujumbe wa Uongozi wa Jumuiya ya Shia Ithnaasheri Tanzania ukiongozwa na Sheikh Mkuu wa Jumuiya hiyo Maulana Sheikh.Hemed Jalala, baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar leo 30-5-2024.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, 

Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameeleza umuhimu wa kutunza 

amani kwa maendeleo na ustawi bora wa watu na Taifa.

Amesema amani na kuwaunganisha watu kuwa kitu kimoja ni chachu ya kujenga ustawi bora wa jamii na kukuza uchumi wa nchi.

Alhaj Dk. Mwinyi ameyasema hayo Ikulu Zanzibar, alipokutana na Sheikh Mkuu wa Jumuiya ya Waislamu wa Madhehebu ya Shia, Tanzania ‘TIC’ Maulana Sheikh Hemed Jalala Mwakindenge na ujumbe alioongozana nao.

Alhaj Dk. Mwinyi alisema maendeleo ya nchi hayaji eneo lenye vurugu au vita, yanaboreshwa kwenye utulivu, umoja, usalama na mshikamano wa watu, pia nia rahisi kuyafikia.

Alisema, hata kama hakuna maelewani kwa asilimia zote kwani hakuna jamii isiyo na migogoro lakini isipitilize ikawa tishio kwa amani, walao sehemu kubwa ya jamii iwe na maelewano ndipo mafanikio yanapatikana.

Pia, aliwashukuru viongozi wa dini wa madhehebu yote pamoja na wananchi wa kuendelea kuhubiri na kuiombea nchi amani na mshikamano, vilevile ameendelea kumuomba Mwenyezi Mungu aendelea kuidumisha nchi kwenye amani na utulivu uliopo kwa mafanikio makubwa.

Halkadhalika, ameendelea kuwashukuru viongozi hao wadini wa medhehebu yote kwa kuendelea kuwaombea heri, amani na mafanikio makuwa viongozi na serikali ili kuendelea kukamilisha vyema mipango ya sekali kwa maendeleo ya nchi kwa ujumla.

Naye, Sheikh Jalala amempongeza Rais Dk. Mwinyi kwa kazi nzuri ya maendeleo kupitia sekta mbalimbali ikiwemo mafanikio makubwa yaliyofikiwa kwenye huduma za jamii, ikiwemo maji safi, umeme, elimu na afya, halikadhalika miundombinu ya barabara na mawasiliano.

Kwa upande wake Msemaji wa Jumuia hiyo, Yasmin Aloo pia amepongeza mafanikio makubwa ya maendeleo yaliyofikiwa na awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wake.

Jumuiya ya Waislamu wa Madhehebu ya Shia, Tanzania ‘TIC’, ilisajiliwa tangu mwaka 1992.

IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.